Tuesday, June 16, 2015

LUKUVI ATOA MSAADA WA PIKIPIKI 16 KWA MAKATIBU KATA WA CCM JIMBONI KWAKE

Makatibu kata wa CCM jimbo la Isimani wakiwa wamezunguka pikipiki 16 zilizotolewa na mbunge wao Wiliam Lukuvi kwa ajili ya  kuwasaidia katika shughuli za kila siku
Katibu wa CCM mkoa wa Iringa Hassan Mtenga  akijaribu moja kati ya  pikipiki 16  zilizotolewa na mbunge wa jimbo la Ismani Wiliam Lukuvi kwa makatibu kata wa CCM jimboni kwake kwa ajili ya kusaidia usafiri  ofisi za kata
makatibu kata na katibu wa wilaya  ya Iringa  wakishangilia  wakati katibu wa mkoa wa Iringa Hassan Mtenga akijaribu pikipiki hizo
katibu  wa mbunge wa jimbo la Isimani Bw  Thom Malenga  kushoto akimkabidhi simu 16  zilizotolewa pamoja na pikipiki 16  na mbunge Lukuvi  kwa ajili ya makatibu wa CCM kata
Katibu   wa CCM mkoa  wa Iringa Hassan Mtenga akikabidhi simu kwa katibu kata wa CCM jimbo la Isimani
 Na MatukiodaimaBlog

MBUNGE wa jimbo la Isimani Bw Wiliam Lukuvi emekabidhi msaada wa pikipiki 16  zenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 22 makatibu kata wote 16  wa chama cha mapinduzi (CCM )katika  jimbo hilo la Isimani wilaya ya  Iringa vijijini   ili kuwawezesha kufanya kazi ya chama kiufanisi  zaidi .

Akikabidhi  msaada  huo pikipiki  na simu 16 leo kwa makatibu hao wa kata kwa niaba ya  mbunge Lukuvi ,katibu wa CCM mkoa wa Iringa Bw Hassan Mtenga  alisema kuwa mkoa wa Iringa una  zaidi ya  wabunge wa watano wanaotokana na chama cha CCM  ila hajapata  kuona  mbunge anayewajali makatibu wa chama kama  alivyofanya mbunge huyo wa  jimbo la Isimani na kuwa kufanya  hivyo  ni  kuongeza ushindi wa CCM .

" katika  mkoa  wetu  wa Iringa tunaowabunge wa CCM lakini  toka  wameanza  mbaka wanamaliza  hawajapata  kutoa msaada kama  huo  ila Lukuvi  si tu anaanza leo tuseme ni  muendelezo kwa   ni mara kwa mara amekuwa jirani na chama  kwa  kusaidia  makatibu hao usafiri  wa  pikipiki na kuwa  hii ni mara ya pili anatoa msaada  huo wa pikipiki baada ya  zile za awali  kuchakaa"

Bw  Mtenga  alisema  kuwa Lukuvi amekuwa ni mbunge na kiongozi  wa aina   yake  kwani amekuwa ni msaada mkubwa  zaidi ndani ya chama na hata  serikalini kutokana na utendaji kazi wake na  hivyo mbali ya  kuwa si  wakati muafaka sana ila  yeye kama katibu wa CCM mkoa wa Iringa anatambua mchango mkubwa na heshima kubwa ambayo mbunge Lukuvi ameonyesha ndani ya chama na katika  jimbo lake la Isimani kwa kutekeleza ilani  vizuri na hivyo kuwataka makatibu hao na  wana CCM jimbo la Isimani kuendelea kutoa ushirikiano kwa mbunge wao.

" Mimi  ni katibu  wa CCM mkoa hivyo natamka  wazi  kuwa mbunge   Lukuvi aendelee kuwa mbunge wa  jimbo la Isimani kwani ni mbunge anayetambua changamoto za  watendaji  wake na  wananchi waliomchagua na kuzitatua na ndio jambo ambalo chama kinahitaji kwa  wabunge  wake  kuzifanya "

Katibu  wa CCM wilaya ya Iringa Bw Andrew Kashililika alisema kuwa msaada  huo wa  piki piki katika jimbo la Isimani ni msaada  mkubwa  zaidi kwani hali ya  usafiri kwa makatibu wa CCM kata  bila jitihada za mbunge  huyo hali ya utendaji kazi kwao  ingekuwa ngumu  zaidi.

katibu  huyo  alisema ushindi ambao  CCM iliupata katika uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa CCM kushinda  zaidi ya asilimia 90n katika wilaya  hiyo ya Iringa  vijijini ni wazi katika  uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba mwaka huu CCM kitaibuka na ushindi  wa  kishindo zaidi .

Kwa upande  wake  katibu  wa ofisi ya mbunge Lukuvi Bw Thom Malenga  alisema  kuwa  ofisi ya mbunge  ilipokea barua za maombi kutoka kwa makatibu hao wa CCM kata  kuomba  kupewa  pikipiki mpya  baada ya  zile za awali kuchakaa na  hivyo kukwamisha  utendaji kazi wao .

Alisema  kuwa  baada ya hapo  ndipo  Lukuvi alipoamua  kutafuta  pesa kiasi cha Tsh milioni 26 kwa ajili ya kununua pikipiki  hizo na kuwapa mawasiliano ya simu baada ya  kuwa  sehemu kubwa ya  jimbo  hilo kuwa na mawasiliano ya  simu na kutokana na kuwa na vitendea kazi vya  mawasiliano itawawezesha kufikisha taarifa  kwa haraka katika  makao makuu ya  chama.

Hata  hivyo  aliwataka makatibu kata  hao kujaribu  kuwa waangalifu  katika kutumia pikipiki  hizo ili  kuepuka kuwasababishia ajali kwani bila uangalifu katika matumizi  upo  uwezekano wa badala ya  kufurahia msaada  huo wakaishia  kujutia  majeraha yatakayotokana na wao kutokuwa makini.

Bw  Zacharia Kitule katibu kata  wa CCM kata ya Nyang'oro  akishukuru  kwa niaba ya  wenzake kwa msaada  huo alimpongeza mbunge Lukuvi kwa kuwamsikivu na kutimiza kila anachoahidi kwa  wakati zaidi na kuwa wao kama makatibu kata wapo tayari  kuendelea  kutoa ushirikiano zaidi kwake  ili kuona anaendelea  kuwa mbunge wa  jimbo hilo hadi hapo atakapoamua  kustaafu mwenyewe.

No comments:

Post a Comment