MATUKIO - SIASA

Hili ni toleo maalum la Michuzi Blog kwa ajili ya matukio mbalimbali ya ziada ya kisiasa nchini katika kuendeleza Sera yetu ya Hatuchagui, hatubagui, ataetuzika hatumjui. Karibuni wote

Friday, June 12, 2015


Monica  Mbega  (kulia) akifurahi pamoja na wana CCM Iringa mjini ambao  walijitokeza kumdhamini  kuwa mgombea wa nafasi ya  urais   kupitia CCM
Monica  Mbega  akisisitiza  kuwa hakuna zaidi  yake
Monica Mbega  akizungumza na  wanahabari  mjini Iringa  leo baada ya  kudhaminiwa na wanachama  zaidi ya 33
Mwenyekiti  wa CCM wilaya ya Iringa mjini Abed Kiponza akitoa taarifa ya  idadi ya  wana CCM waliomdhamini Mbega
Mbega  akifurahia  orodha  ya  wana CCM waliomdhamini
Baadhi ya  wadhamini wa  Mbega  Iringa
Kada wa CCM mama Mwalusamba  akimuombea dua Monica Mbega
Monica Mbega akionyesha orodha ya  wadhamini  wake
Wadhamini wa Mbega  Iringa

Hata  mimi nimechukua fomu ya  Urais :Naibu  meya  wa Manispaa ya  Iringa ambae ni diwani  wa kata ya  Ilala Bw  Gervas Ndaki akifurahia kushika mkoba  wenye fomu ya  CCM ya  kuomba kuwa mgombea  wa nafasi ya  Urais  wa Jamhuri ya  Muungano  wa Tanzania ,fomu ya Monica Mbega  baada ya mgombea  huyo  kufika mjini Iringa  kusaka  wadhamini 30

 Na  Matukiodaima Blog
WAKATI mbio za makada  wa chama  cha mapinduzi (CCM)  waliotia nia ya  kuomba  kuteuliwa  kuwa wagombea wa nafasi za urais zikiendelea  kushika kasi kwa  kila mgombea kutumia mbinu yake ya  kuwafikia wana CCM kuomba udhamini , aliyekuwa mbunge wa  jimbo la Iringa mjini Monica Mbega leo  ameingia wilaya ya Iringa mjini mkoani hapa  kuomba udhamini na kupata  wajumbe 33  huku akiwataka  watanzania kutoaminishwa na mbwembwe  za  watia nia wenzake wanazofanya mikoani na  kuwa yeye ndie Rais wa awamu ya tano baada ya Dr Jakaya Kikwete  na  kuwataka  watia  nia wenzake wamuunge mkono.

Mbega ambae  alilazimika  kusubiri wajumbe 30   wa  kumdhamni  kwa  zaidi ya masaa manne katika ofisi ya CCM wilaya ya  Iringa  mjini  alitoa kauli  hiyo wakati  akizungumza na  wanahabari juu ya safari  yake  hiyo ya  kutaka  kwenda Ikulu na kudai  kuwa amelazimika  kuzuia  viongozi  wa CCM wilaya ya  Iringa kutomuandalia  mbwembwe  zozote wala wapambe wa kumshangilia  wakati  wa safari  yake  hiyo ya  kutafuta  wadhamini.

Alisema  kuwa kuwa anamtegemea  Mungu  zaidi katika  safari yake  hiyo ya kwenda Ikulu na ndio maana  hakupenda  kuweka makisio ya gharama  za safari nzima ya mchakato huo wa kuelekea  kupokea kijiti kwa Rais Dr Kikwete na  hivyo ndio  sababu ya  yeye  kuzunguka  bila ya mpambe zaidi ya dereva  anayemuendesha pekee.

" Naomba  niwaelezeni  wazi  kuwa sina mgombea  wa  kumuunga mkono kati ya  wote  waliojitokeza  zaidi ya 30 kwani naamini  kuwa namba   moja kati ya  wote  hao waliojitokeza ni  Monica Ngenzi Mbega   ninasema   hivyo  kwa  kuwa  nchi ya  sasa inahitaji mwamanke kuongoza  kwani  mwenye  kuweza  kuvunja makundi ni mwanamke sio mwanaume tena .....mwanamke ni mwepesi  wa  kusamehe  sio mtu wa makundi hivyo kama hivyo  ndivyo ukitanguliza  upendo makundi hayatakuwepo ila  wapo  wenye visasi vya kutoka mwaka 2005 ila sio mimi ....mimi nimetanguliza upendo  zaidi....mimi  ni mama nitaiunganisha  nchi na  changamoto  inayomkabili Rais wa awamu ya tano ni  jinsi na kuiunganisha  nchi na mimi ndie pekee  wa kuunganisha nchi hii"

Alisema  kuwa  iwapo  watanzania  wataunganishwa  kuwa  wamoja kuna  uwezekano  wa nchi  kuachana na utegemezi na hivyo  wananchi  wake kuwa  wamoja na  kuweza kushiriki kujiletea maendeleo yao  chini ya rais wao Mbega .

Hivyo  alisema  kuwa iwapo chama  chake  kitamteua  na watanzania  wakamchagua  na  kuingia Ikulu  wategemee Tanzania  mpya  yenye amani ,upendo na mshikamano na uchumi  bora  kwa  kila mtanzania  kuongeza pato  binafsi .

Mbega  alisema  kuwa tayari  Rais wa nchi  Dr  Kikwete  amepata  kuueleza  umma kuwa misaada ambayo  nchi  inapata  kutoka kwa  wahisani mingine ina masharti magumu  na ndio maana  ya baadhi ya miradi kushindwa  kukamilika kwa  wakati na  kuwa iwapo yeye ataingia  Ikulu atajaribu kukwepa misaada  hiyo na  kulijenga Taifa  linalojitegemea lenyewe  ili kuto kuwa na miradi isiyo kamilika kutokana na masharti magumu ya  wahisani .

Alisema  kuwa  kikubwa  kilichomsukuma kuchukua  fomu  ya  kutia nia kuomba  kuteuliwa  kuwania Urais ni uzalendo  wake  katika Taifa wenye shauku  la  kuliongoza Taifa la Tanzania kama mwanamke  wa kwanza  toka  nchi ipate  uhuru  wake mwaka 1961 bila ya  kuongozwa na mwanamke na  kudai kuwa hakuna  mgombea  wa CCM ambae anajambo lake  binafsi la  kufanya  zaidi ya kutekeleza  ilani ya uchaguzi ya CCM.

"Falsafa  yangu ni kusahihisha  changamoto zinazoonekana  katika  kutekeleza  ilani hatujaweza  kufanikiwa hili ....mheshimiwa Rais Dr Kikwete  tunaona jinsi anavyotekeleza ilani katika  sekta  mbali mbali ila  utasikia  katika  vikao  vya kamati  kuu  wakati akitoa taarifa ya  utekelezaji  kuwa kuna changamoto mbali mbali ambazo zimekwamisha  utekelezaji wa ilani hivyo  mimi nitaanzia kutekeleza  changamoto kwanza .....kwani bajeti  inayotengwa ndio inapaswa  kusimamiwa  kwanza  mwelekeo mzima  wa serikali yangu ni  kuona tunapata Taifa la watu  wanaojitegemea wenyewe"

Katika  hatua nyingine Mbega ambae aliangushwa nafasi ya  ubunge  mwaka 2010 na mbunge Peter Msigwa (Chadema)  alisema  kuwa bado ana nguvu  ya  kurudi  kugombea ubunge  jimbo la Iringa mjini na kumshinda mbunge  wa sasa mchungaji Msigwa kwani bado nguvu  za  kurejesha  jimbo hilo  CCM anazo japo hana mpango wa ubunge zaidi ya  kutimiza dhamira yake ya  kuingia Ikulu kama Rais aliyokuwa nayo toka mwaka 2005 na  alishindwa  kuingia mwaka 2010 kwa  kumheshimu Rais Dr  Kikwete pekee ila  sasa ni zamu  yake .

Pia  alisema   CCM bado ina nguvu zaidi katika  jimbo la Iringa mjini na Tanzania kwa ujumla na iwapo  suala la upendo  likawatangulia  watia nia wote pale  wanapokosa  kuteuliwa kuungana kwa upendo  kumuunga mkono aliyeteuliwa kamwe suala la wapinzani  kushinda  litabaki  kuwa ni ndoto.
 
Wakati  huo  huo huo mgombea  huyo amewaacha hoi wanahabari  waliofika kumsikiliza baada ya  kudai kuwa waandike majina  yao kamili na namba  zao  za  simu ili kuja  kuwakumbuka katika ufalme  wake pindi atakapoingia Ikulu 









Posted by MICHUZI BLOG at Friday, June 12, 2015
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

Contributors

  • KILINGE CHA HABARI BLOG
  • MICHUZI BLOG
  • MtaaKwaMtaa

Blog Archive

  • ►  2019 (1)
    • ►  December (1)
  • ►  2016 (3)
    • ►  December (1)
    • ►  March (1)
    • ►  January (1)
  • ▼  2015 (258)
    • ►  November (1)
    • ►  October (49)
    • ►  September (85)
    • ►  August (18)
    • ►  July (40)
    • ▼  June (65)
      • Dkt MUSA MDEDE apata Baraka za kuwa mbunge wa jimb...
      • LOWASSA AHITIMISHA ZIARA YA KUTAFUTA WANACCM WA KU...
      • WanaCCM 78, 500 wa Mkoa wa Pwani wamdhamini Mh. Lo...
      • HARAKATI ZA NYALANDU KUSAKA ADHAMNI JIJINI ARUSHA LEO
      • MAFURIKO YA LOWASSA YAHAMIA JIJINI DAR, AKOMBA UDH...
      • CHADEMA MOSHI VIJIJINI WARUDISHA FOMU ZA KUWANIA U...
      • MCHAKA MCHAKA WA LOWASSA WATINGA MANYARA LEO, APAT...
      • NASSARI AMALIZA MIKUTANO YA KUHAMASISHA WANANCHI K...
      • LOWASSA APATA UDHAMINI WA KISHINDO JIJINI ARUSHA L...
      • NYALANDU APATA WADHAMINI MKOANI KILIMANJARO
      • MAKAMU WAPILI WA RAIS WA ZANZIBAR BALOZI SEIF ALI ...
      • Ziara ya January Makamba Kusaka Wadhamini Shinyanga
      • KINANA AANZA ZIARA YAKE MWANZA KWA KISHINDO
      • LOWASSA AZIDI KUPATA MAPOKEZI MAKUBWA KILA ANAKOKW...
      • GEITA NA MARA WAJITOKEZA KWA WINGI KUMDHAMINI WAZ...
      • Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania Addo Novembe...
      • MH. LOWASSA APATA UDHAMINI WA WANACCM 69,462 KATIK...
      • January Makamba atua Jiji la Mwanza kusaka Wadhamini
      • WAZIRI BERNARD MEMBE AWASILI BUKOBA KUSAKA WADHAMINI
      • KINANA APIGA KAZI BUSANDA NA MJI MDOGO WA KATORO L...
      • January apata wadhamini Tabora, Kwao Tanga Apata ...
      • WANACCM 53,156 WAMDHAMINI MH. LOWASSA JIJINI MBEYA...
      • Dkt Asha-Rose Migiro apata wadhamini mkoani Kigoma...
      • NASSARI AENDELEA KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA K...
      • KILIMANJARO YAVUNJA REKODI YA UDHAMINI KWA MH. LOW...
      • MAKONGORO NYERERE AKAMILISHA ZOEZI LA KUTAFUTA WAD...
      • WAZIRI BERNARD MEMBE AUTINGISHA MKOA WA MANYARA AP...
      • KINANA AINGIA NYANG'HWALE KUENDELEA NA ZIARA YAKE ...
      • PROF MWANDOSYA ASEMA MWAKA 2005 NILIKUWA WA TATU M...
      • TASWIRA MBALIMBALI ZA MH. LOWASSA AKISAKA UDHAMINI...
      • ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA NDANI YA ...
      • WAZIRI MKUU APATA WADHAMINI 9,141 KATAVI
      • MTWARA WAJITOKEZA KWA WINGI KUMDHAMNINI DKT. MAGUFULI
      • LUKUVI ATOA MSAADA WA PIKIPIKI 16 KWA MAKATIBU KAT...
      • LOWASSA AWEKA REKODI MPYA, SINGIDA APATA WADHAMINI...
      • MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA WAELIMISHA JUU YA VIPOD...
      • ZITTO KABWE AWAHUTUBIA WAKAZI WA MKOA WA KAGERA KW...
      • PROFESA MARK MWANDOSYA AENDELEA KUSAKA WADHAMINI M...
      • MGOMBEA URAIS, DKT. MOHAMMED GHARIB BILAL, ARUDI...
      • MAPOKEZI YA MH. LOWASSA MJINI BUKOBA HAYANA MFANO,...
      • LOWASSA APATA UDHAMINI WA KISHINDO KATIKA MIKOA YA...
      • M/KITI WA KAMATI YA MAHUSIANO YA JAMII UVCCM JUMA ...
      • ACT Maendeleo yazindua Azimio la Tabora
      • DKT. MAGUFULI ATAPA WADHAMINI KATIKA MIKOA YA UNGU...
      • LOWASSA APATA UDHAMINI WA KISHINDO KATIKA MIKOA YA...
      • DK. MALECELA ASAKA WADHAMINI KATIKA KUGOMBEA NAFAS...
      • WASIFU WA BERNARD KAMILIUS MEMBE
      • MH. LOWASSA ATUA KIGOMA LEO, AZOA WADHAMINI 11,250
      • MH. LOWASSA AZIDI KUVUNJA REKODI, APATA WADHAMINI ...
      • PINDA ACHUKUWA FOMU YA KUWANIA UTEUZI WA CCM KUGOM...
      • MAKAMBA AITIKISA RUVUMA, UDHAMINI WA WATU 3550 WAV...
      • More 22 of 75 DKT.MAGUFULI AZIDI KUPATA WADHAMI...
      • DKT.MAGUFULI AZIDI KUPATA WADHAMINI KATIKA MIKOA Y...
      • Monica  Mbega  (kulia)...
      • MAKAMBA: TUEPUKE USHABIKI NA KUCHAFUANA, TUTAUA CHAMA
      • UN YATAKA KUWEZESHWA ZAIDI KWA SERIKALI ZA MITAA.
      • Makamba: Tuepuke ushabiki na kuchafuana, tutaua chama
      • MH. BERNADY MEMBE APOKELWA KWA KISHINDO MKOANI RUV...
      • WASIRA AWAIMIZA WAKAZI WA MTWARA KUWEKEZA KATIKA U...
      • MAKAMBA AVUNJA REKODI YA MAPOKEZI NA UDHAMINI IRINGA
      • LOWASSA ATIKISA SHINYANGA, WANA CCM ZAIDI YA 7000 ...
      • LOWASSA APATA WADHAMINI ZAIDI YA ELFU SABA MKOANI ...
      • WAZIRI BERNARD MEMBE AFUNGUA MKUTANO MKUU WA UMOJA...
      • Makamba Avunja rekodi ya mapokezi na wadhamini mko...
      • MAMBO MATATU USIYOYAJUA JUU YA MWENYEKITI WA BODI ...
Picture Window theme. Powered by Blogger.