Sunday, June 14, 2015

DK. MALECELA ASAKA WADHAMINI KATIKA KUGOMBEA NAFASI YA URAIS

 Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti Magonjwa ya Binadamu Dk. Mwale Malecela  pichani kabla ya kuingia  katika chumba cha habari katika Redio ya Mwambao iliyopo Tanga eneo la Kange ndani ya Kiwanda cha Tanga Fresh ambaye ni mtoto wa Makamu wa zamani wa Chama cha Mapinduzi (CCM)  John Malecela ni miongoni mwa wana CCM ambao wamejitosa kugombea urais kupitia CCM. Dk. Mwale katika maisha yake mengi kwa zaidi ya miaka20 amekua mtumishu katika Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR)  ambako alianza kazi akiwa kijana na akapanda hadi kuwa mtafiti mkuu na baadaye akateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu, licha ya kukulia katika familia ya mwanasiasa. 
 Dk. Mwale Malecela akizungumza na wananchi kupitia kituo cha Mwambao Radio
 Dk. Mwale Malecela (kulia) akizungumza na wananchi kupitia kituo cha Mwambao Radio kilichopo Tanga eneo la Kange ndani ya Kiwanda cha Tanga Freshi, kushoto ni mtangazaji wa zam Jonas Msangi
Dk. Mwale Malecela katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa  kituo cha Mwambao Radio.(PICHA NA KHAMISI MUSSA) Mmiliki wa UJIJIRAHAA BLOG.

No comments:

Post a Comment