Thursday, September 17, 2015

NITATUMIA TOCHI KUFICHUA MAFISADI - CHUMI

Mgombea  ubunge  jimbo la Mafinga Bw  Cosato Chumi kulia akisalimiana na mmoja kati ya  wapiga kura  wake
 Mgombea  ubunge  jimbo la Mufindi Kaskazin Bw Mahamudu Mgimwa  akiwahutubia wananchi  wakati wa mkutano wa Chumi
 Mjumbe wa NEC Mufindi Marcelina Mkini  akiomba kura  za CCM
 Mjumbe wa NEC  Iringa Mahamudu Madenge akizungumza na wananchi wa jimbo la Mafinga


MGOMBEA  Ubunge wa Jimbo la Mafinga Bw. Cosato Chumi (CCM) amewataka wananchi wa jimbo hilo kuwa na iamani  na kuwa wakimchagua atahakikisha anamulika kwa kutumia tochi ubadhilifu katika sekta za elimu, afya, kilimo, barabara, maji na kuhakikisha kuwa hakuna fedha ambazo zitatolewa na serikali kuleta maendeleo kwa wananchi zitaliwa na watendaji ndani ya jimbo la Mafinga.
 
Hayo ameyasema jana wakati alipokuwa akijinadi kwa wananchi wa jimbo la Mafinga katika Mtaa wa Bomani ambapo pia ulifanyika uzinduzi wa kampeni za udiwani katika kata hiyo na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu pamoja na madiwani wote ambao wametangaza nia ya kuwania nafasi zao katika jimbo hilo la Mafinga Mjini.
 
Bw. Cosato Chumi alisema kuwa wananchi wa jimbo la Mafinga ni mashahidi wa shida zinazowapata na kuwakera wananchi ndani ya jimbo la Mafinga Mjini ambapo alisema kuwa Hospitali ya wilaya kutokana na kuzidiwa  na wagonjwa atahakikisha kuwa anapigania ili kila kata kuwe na zahanati na katika tarafa za ndani ya Mafinga kujengwe kituo cha Afya ili kupunguza msongamano wa wagonjwa.
 
Bw. Chumi aliongeza kuwa atapigania ili madawa na mahitaji yote ya msingi kwa wananchi hususani wagonjwa kuwa yapatikane na kuhudumia wananchi ambao kwa sasa kutokana na mlundikano mkubwa wa wagonjwa katika Hospitali ya wilaya wagonjwa wanapoteza muda mwingi katika kutafuta matibabu ya afya zao na familia zao.
 
“Nitahakikisha kuwa pesa zote za Umma za maendeleo zinasimamiwa kikamilifu na hakuna ufujaji wa aina yoyote ile ambao utatokea na kuongeza kuwa fedha zote zitakazotolewa ndani ya mfuko wa jimbo, pesa za serikali za maendeleo pamoja na miradi mbalimbali zitamulikwa kwa umakini ili zitekeleze shughuli ambayo imelengwa”, alisisitiza Bw. Chumi.
 
Alisema kuwa endapo viongozi wanategemea sana utendaji wa kazi na shughuli za viongozi kutokana na kuwepo kwa umoja na mshikamano ambapo alisema kuwa shule za sekondari zitahakikisha kuwa zinaendelezwa kila kata na kuwahakikishia wananchi hususani watoto wao wanapata elimu sahihi.
 
Aidha, alisema kuwa mabweni katika shule za sekondari yatahakikisha kuwa yanajengwa kwa malengo ya kuhakikisha kuwa wanafunzi wanatulia shuleni na kusoma kwa utulivu ambapo alisema kuwa sekta ya elimu inatakiwa ipewe kipaumbele ili watanzania wote waelimike na kuwezeshwa kujitegemea na kujiajiri na kuajiriwa na sekta za binafsi na serikali kwa manufaa ya kukuza uchumi ndani ya nchi.
 
Akizungumzia suala la kushughulikia usalama, Bw. Chumi alisema kuwa atahakikisha kuwa anapigania kila kata ndani ya jimbo la Mafinga linajengewa kituo cha Polisi ili kuwasaidia wananchi kulinda usalama na mali zao, kuwasaidia wananchi endapo watahitaji misaada ya haraka kutoka kwa sekta ya ulinzi wa jeshi la polisi ikiwemo mwananchi akipata ajali, akiibiwa, akivamiwa na kupata misukosuko ya aina yoyote ile ambayo itahitaji jeshi la polisi kuingilia kati kushughulikiwa kwa haraka.
 
  JENGENI IMANI NA CCM KWA MAENDELEO ZAIDI - JIMSONI MHAGAMA
 Katibu  wa CCM wilaya ya  Mufindi, Jimsoni Mhagama 
KATIBU wa CCM wa wilaya ya Mufindi Bw. Jimson Mhagama amesema kuwa chama  cha mapinduzi (CCM ) kitaendelea  kuongoza kwa kuzingatia uadilifu, , amani, upendo, utulivu na kuleta maendeleo kwa wananchi wake  hivyo  kuwataka  wananchi kuchagua cheni nyenye msimamo wa kuwa na diwani, mbunge na rais wa CCM ili  kuendelea  kuwaletea maendeleo .
Bw. Mhagama aliitoa kauli  hiyo  jana alipokuwa akihutubia wananchi katika mkutano  wa  kampeni za udiwani wa kata ya Bomani kwa  kumnadi mgombea wa kata hiyo  Bw. John Chota  ,kuwa  wananchi waanze kumuunga mkono diwani, na mbunge anayegombea wa CCM Bw. Cosato Chumi kumchagua kuwa mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini pamoja na kuelekeza kura zote  kwa Mgombea wa Urais dkt. John Magufuli.
“Uongozi wowote wenye cheni moja ya kutoka chama kimoja ndiyo unaoweza kuleta maendeleo na hivyo ninawaomba kura zenu mzielekeze kwa diwani wetu John Chota, Mbunge wetu Bw.  Cosato Chumi pamoja na Rais wetu dkt. John Pombe Magufuli ili kuunda cheni moja ya mshikamano na kutokana na uwepo wa cheni hiyo kutakuwa na mfumuko sahihi wa maendeleo kwa wananchi katika sekta zote zikiwemo za elimu, kilimo, afya, barabara, ujasiliamali, kutunza mazingira, ajira kwa vijana na uwezeshaji wa akina mama”, alisema Bw. Jimson Mhagama.
Alisema kuwa kutokana na kuwepo kwa cheni moja ya kimaendeleo uongozi wa awamu ya Tano utakapoingia madarakani utahakikisha kuwa shule zote za sekondari zinapatiwa umeme, kuendeleza ujenzi wa maabara, kuhakikisha zinapatiwa walimu wa kutosha  na kuongeza kuwa elimu itatolewa bure kuanzia shule za msingi hadi sekondari kwa ajili ya kuhakikisha kuwa watanzania  walio wengi ambao ni vijana wanaelimika na kunufaika na matunda ya nchi yao.
Aidha, alisema kuwa mara baada ya uchaguzi Jimbo la Mafinga litahakikisha kuwa linajenga stendi kubwa ya kisasa ya mabasi yaendayo mikoani ambayo yanapita katika Mji wa Mafinga  ambapo alisema kuwa ujenzi wa stendi hyo utagharimiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa LAPF ambapo stendi hiyo inatarajia kugharimu zaidi ya shilingi Bilioni 3.5 na kuongeza kuwa utendaji huo utakwenda sambamba na wananchi kuchagua cheni moja ya CCM na siyo kuleta mchanganyo wa wagombea.

No comments:

Post a Comment