Friday, September 18, 2015

MAMA SAMIA, MIKINDANI NA MAFIA JANA.

 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia umati wa wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika jana, Septemba17, 2015, katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara.
  Wananchi wakimshangilia Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipohutubia mkutano wa kampeni kwa ajili ya Jimbo la Mtwara mjini, uliofanyika katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara jana, Septemba 17, 2015.
  Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akipokea Wanachama waliohamia CCM, kutoka vyama vya CUF na Chadema, wakati wa mkutano wa kapnei uliofanyika jana, Septemba 17, 2015 katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara.
 Kada wa CCM, Mtela Mwampamba akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika jana, Septamba 17, 2015 katika mji mdogo wa Mikindani, Jimbo la Mtwara Mjini.

 Msanii wa Bongo Movie, Snura akitumbuiza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Septemba 17, 2015 katika mji mdogo wa Mikindani mkoani Mtwara.
 Vijana wakiungana na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan kuishangilia CCM, baada ya kuwapokea kutoka vyama vya CUF na Chadema katika mkutano wa kampeni uliofanyika jana, Septemba 17, 2015.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Mafia mkoani Pwani, jana, Septemba 17, 2015.
 Aliyekuwa Mbunge wa Mafia ambaye pia aliingia katika kinyan'ganyiro cha kuomba ridhaa ya CCM kuwania tena ubunge wa jimbo hilo, Abdulkarim Shah, akimnadi Mgombea wa Ubunge wa jimbo hilo, Mbarak Dau, katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika katika Kisiwa hicho cha Mafia.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimpongeza Kada wa CUF, Mohamed Albadawi, baada ya kutangaza kuhamia CCM katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Mafia mkoa wa Pwani. Albadawi awali alikuwa Mgombea Ubunge katika jimbo hilo kwa tiketi ya CUF baada ya kuongoza katika kura za maoni, lakini baadaye akaenguliwa na chama hicho na kupachikwa, Shomari Kimbau ambaye alihamia CUF baada ya kushindwa katika kura za maoni za CCM.
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia suluhu (Kushoto), akishiriki kucheza muziki wa taarab uliokuwa ukitumbuizwa na nguli wa muziki huo, Mzee mwishoni mwa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Mafia mkoa wa Pwani. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments:

Post a Comment