Tuesday, September 22, 2015

Mama Samia Suluhu Hassan Amnadi Dk. Magufuli Wilaya za Korongwe na Lushoto


Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo mjini Korogwe, Mkoa wa Tanga.
Mgombea mwenza nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na wasanii na wananchi wengine alipokuwa akiwasili katika viwanja vya Shule ya Msingi Mazoezi leo Mjini Korogwe ambapo alifanya mkutano wa kampeni.
Mgombea mwenza nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu Hassan (kulia) akiwapokea baadhi ya wanachama wapya waliojiunga na CCM katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo Korogwe. Jumla ya wanachama 25 walijiunga na CCM katika mkutano huo.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo mjini Korogwe, Mkoa wa Tanga.
Baadhi ya wasanii waigizaji, Wema Sepetu (kulia) na Bibi Mwenda wakizungumza na WanaCCM na wananchi katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza kuwashawishi waichague CCM kutokana na mazuri mengi iliyowafanyia wasanii.
Mgombea mwenza nafasi ya urais wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu Hassan (kulia) akimtambulisha na kumuombea kura mgombea ubunge wa Jimbo la Bumbuli, January Makamba (katikati) katika mkutano wa hadhara wa kampeni wa mgombea mwenza uliofanyika Lushoto Jimbo la Mlalo. Kulia ni mgombea wa ubunge Jimbo la Lushoto, Shaban Shekilindi.
Mgombea Ubunge Jimbo la Korogwe Mjini, Mary Pius Chatanda akizungumza na wanaCCM na wananchi wa jimbo hilo walipojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza leo viwanja vya Shule ya Msingi Mazoezi.

Mgombea Ubunge Jimbo la Korogwe Mjini, Mary Pius Chatanda akizungumza na wanaCCM na wananchi wa jimbo hilo walipojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza leo viwanja vya Shule ya Msingi Mazoezi kunadi sera za CCM, huku mgongoni akiwa amebandika kipeperushi cha mgombea urais wa CCM, Dk. John Magufuli.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Profesa 'Maji Marefu' akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara wa kampeni za mgombea mwenza uliofanyika Korogwe Mjini leo.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo mjini Korogwe, Mkoa wa Tanga.

Mwenyekiti wa CHADEMA Kata ya Kwagunda, Salehe Abdullah (kushoto) akizungumza mara baada ya kujiunga na CCM leo kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza na kukikimbia chama chake cha CHADEMA.
Mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wanaCCM na wananchi wa jimbo la Korongwe Mjini walipojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea huyo leo kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Mazoezi.
Baadhi ya wananchi wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan eneo la Mombo ili asikilize kilio na changamoto zao kabla ya kuendelea na safari kwenda kuhutubia mkutano wa kampeni Wilaya ya Lushoto.
Baadhi ya wananchi wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan eneo la Mombo ili asikilize kilio na changamoto zao kabla ya kuendelea na safari kwenda kuhutubia mkutano wa kampeni Wilaya ya Lushoto.
Sehemu ya wananchi  na wanaCCM wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan eneo la Soko la Soni Lushoto ili asikilize kilio na changamoto zao hasa akinamama kabla ya kuendelea na safari kwenda kuhutubia mkutano wa kampeni Wilaya ya Lushoto.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza mgombea mwenza huku wakiendelea na biashara zao sokoni hapo.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza mgombea mwenza huku wakiendelea na biashara zao sokoni hapo.
Sehemu ya wananchi  na wanaCCM wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan eneo la Soko la Soni Lushoto ili asikilize kilio na changamoto zao hasa akinamama kabla ya kuendelea na safari kwenda kuhutubia mkutano wa kampeni Wilaya ya Lushoto.
Mgombea ubunge wa Jimbo la Bumbuli, January Makamba (kushoto) akibadilishana jambo na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Lushoto, Balozi Abdul Mshangama leo katika Jimbo la Mlalo.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo katika Jimbo la Mlalo, Lushoto.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mlalo, Shaban Omar Shekilindi akizungumza na wapiga kura wake jimboni Mlalo.
Mgombea ubunge Jimbo la Bumbuli, January Makamba akizungumza na umati katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza, Makamba akizungumza aliwaomba wananchi wasikipe kura chama cha Chadema na ushilika wao wa UKAWA kwani wapo kwa ajili ya mabadiliko ya nafsi zao na si vinginevyo.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo katika Jimbo la Mlalo, Lushoto.
Mgombea mwenza, Bi. Samia Suluhu (katikati) akimtambulisha mgombea ubunge wa Jimbo la Lushoto, Shaban Shekilindi.
Mgombea mwenza, Bi. Samia Suluhu Hassan (kushoto) akimtambulisha Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mlalo, Shaban Omar Shekilindi alipokuwa akizungumza na wapiga kura wake jimboni Mlalo.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com



No comments:

Post a Comment