Saturday, September 19, 2015

CHIKU ABWAO: HERI YA MONICA MBEGA WA CCM KULIKO MCHUNGAJI MSIGWA WA CHADEMA NAOMBA NICHAGUENI MIMI SAFARI HII

MGOMBEA  Ubunge wa jimbo la Iringa Mjini kupitia ACT Wazalendo Bi Chiku Abwao(pichani) amesema heri ya miaka mitano ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Mobica Mbega ( CCM) kuliko miaka mitano ya Mchungaji Peter Msigwa ( Chadema)hivyo ametawa mwaka huu wananchi kumchagua yeye

Akizungumza katika mkutano wake wa kampeni za Ubunge jana  kata ya Kihesa alisema iwapo atakuwa mbunge wao atahakikisha anakuwa mbunge wa mfano wa kuwaletea maendeleo sahihi.

Kwani alisema kuwa historia ya jimbo hilo mwaka 1995 walichagua NCCR mageuzi ambapo Bw Mfalamagoha Kibasa kuwa mbunge ila baada ya kushindwa kutekeleza ahadi zake mwaka 2000 walimchagua Monica Mbega ( CCM) ambae kipindi cha kwanza alifanya Kazi vizuri na mwaka 2005 wananchi walimchagua tena ila hakuweza kufanya Kazi ndipo walipomchagua Mchungaji Peter Msigwa( Chadema) ambae hajafanya Kazi yoyote.

Hivyo  alisema  kwa  sasa imani yake  juu ya  wanaume  kuwa  wabunge  katika   jimbo  hilo haipo  tena kwani hawana nia ya  kweli ya  kuwatumikia  wananchi na  kudai kuwa  iwapo  mbunge  aliyemaliza  muda  wake mchungaji Msigwa angetekeleza ahadi  zake vema  leo asingesimama kugombea  ubunge bali  angemuunga  mkono mbunge   huyo ili  aendelee  kwa  kipindi  cha  pili  ila kwa  kuwa hakuna jipya  alilolifanya hana imani nae na  hivyo ni  wakati wa  wananchi wa  jimbo  hilo  kuwapima wagombea  wengine waliojitokeza nje  ya mbunge  huyo .

Alisema ahadi  za  mbunge  aliyemaliza muda  wake  zilikuwa zaidi ya 14  ikiwemo ya  kuwawezesha wananchi  waliojiunga katika  vikundi  kupatiwa  mitaji ya  kuanzisha  biashara  kwa  wakati  huo  alisema  yeye  si mbunge  wa  kutoa pesa bali atawawezesha  kiuchumi kwa  kuwapa nyavu  (mitaji) ila baada ya  kuwa mbunge alianza  kuwasema  vibaya  wananchi kwa kudai yeye  si mbunge wa  kutoa  pesa (ATM)pia  aliahidi  ujenzi  wa  soko la kisasa  Kihesa  na  kumweka mwanasheria  katika  ofisi  yake  ila hadi  sasa hakuna alichofanya na  akikumbushwa  hukimbilia  kujenga  chuki na  kila mtu .

Bi  Abwao  ambae  amepata  kuwa  mjumbe wa kamati  kuu ya Chadema  Taifa na  mbunge  wa viti maalum  mkoa  wa Iringa  kupitia Chadema  alisema  kuwa hali ya chadema na UKAWA  kwa  sasa  imepoteza mwelekeo na  chadema kugeuka ni  chama  cha kutetea  mafisadi   tofauti na  iliyokuwa awali kuwa chama cha  kupinga  ufisadi .

Hivyo  alisema  sababu ya  kukihama  chama  hicho na  kujiunga na ACT  wazalendo ni kutafuta  chama cha  upinzani makini ambacho atawatumikia wananchi  bila ya kuwajengea maswali kama  ilivyo  hivi  sasa kwa  mgombea  wa Chadema Iringa mjini mhungaji Msigwa ambae alikuwa mbele  kupinga ufisadi na hata  kusema  wanaomuunga mkono aliyekuwa  waziri  mkuu Edward  Lowassa ambae ni mgombea wa Chadema kwa  sasa wakapimwe akili  zao .

Alisema Chadema  kwa  sasa  imekuwa ni  chama  cha kupiga  dili akiwemo  aliyekuwa  mbunge wa  jimbo hilo Mchungaji Msigwa ambae leo kati ya maswali magumu ambayo anahojiwa  na  wapiga  kura  wake ni  juu ya kauli  yake  dhidi ya wale  wanaomuunga mkono  LOwasa  kutakiwa  kupimwa akili  zao.

Akielezea  kuhusu  sera  zake  kwa  wananchi  wa  jimbo la Iringa mjini iwapo  watamchagua  kuwa mbunge  wa  jimbo  hilo atahakikisha anautumia  vema  mfuko  wa  jimbo kwa  kuwasaidia  wazee ,vijana na  wanawake  kuwa na  vikundi  vya kiuchumi tofauti na  ilivyokuwa awali miaka  mitano iliyopita  kwa  mfuko  huo kushindwa  kufanya kazi  yoyote.

Pia  kuhakikisha  anaibana  serikali  ili vijana  kupewa mikopo  nafuu na  kuzuia posho kwa  watumishi  wa umma ambazo  zimekuwa  zikikwamisha maendeleo katika  jimbo  hilo .

No comments:

Post a Comment