Monday, September 28, 2015

CHOPA YA CCM YATUA MANYARA,MWIGULU NCHEMBA AENDELEA KUKUSANYA KURA ZA CCM

Mwigulu Nchemba mmoja ya wajumbe 32 wa timu ya Ushindi ya Chama cha Mapinduzi akisalimiana na Wananchi wa Karatu Mjini jioni ya leo alipofika kwaajili ya Kuomba kura kwaajili ya Rais,Mbunge na Madiwani wa Chama Cha Mapinduzi.
Sehemu ya Wananchi wa Karatu Mjini waliofika Uwanjawa Mazingira Bora kusikiliza Mkutano wa hadhara wa Mwigulu Nchemba.Mwigulu Nchemba akitoa darasa kwa Wananchi wa karatu kuhusu biashara ya Kumuacha Dr.slaa na kumpatia Edward Lowassa aliyehamia kutoka CCM.Dr.slaa aliyetumia Jasho na Damu kuuimarisha Upinzani wenye meno,Hii leo ameondolewa kwakuwa DILI imewekwa mezani ili Mtu mwenye kashafa mbalimbali chafu aweze kuwania Urais.Kwaaina ya Mgombea waliosimamisha UKAWA,Mwigulu amesema itakuwa rahisi sana kwa Magufuli kushinda kwa asilimia kubwa sana ya Kura.Wananchi wa Mbulu Vijijini wakisikiliza Mkutano wa Mwigulu Nchemba wakati akinadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi.Mwigulu Nchemba akisalimiana na Wananchi wa BashinetMbulu Vijijini wakati alipokwenda kumuombea Kura Rais Mtarajiwa J.Pombe Magufuli na kuwanadi Madiwani na Wabunge wanaotoka Mkoa wa Manyara.Mwigulu Nchemba akiwasili Dongobesh kuzungumza na Wananchi kwenye Mkutano wa kampeni wa Chama cha Mapinduzi.Mwigulu NChemba akimnadi Mbunge mtarajiwa wa Jimbo Jipya la Mbulu Vijijini Ndg.Flatei hii leo wakati wa mkutano wa kampeni kata ya Dogobesh.Wananchi wa Dongobesh wakionesha ishara ya kuunga mkono Ilani ya CCM,Na kwamba wapotayari kumchagua Magufuli kwenye nafasi ya Urais,Flatei kwenye Ubunge na Madiwani wa CCM.Mwigulu Nchemba akiwasili Mbulu Mjini kwenda kuzungumz na Wananchi.Mwigulu Nchemba akizungumza na wananchi wa Mbulu Mjini hii leo,Amewaomba kuwa mabalozi kwa watu wote kuhusu Ubora wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi na Ubora wa Wagombea wa CCM kwa ngazi zote,"Kila mmoja ajitoe kuwa balozi wa kuhamasisha wananchi wanachagua CCM kwa ngazi zote kwakuwa CCM ndio chama chenye ilani bora na inayotekelezeka.Ndani ya Ilani ya CCM kunamaswala ya kimaendeleo hususani Ujenzi wa Barabara ya kutoka Bareda hadi Mbulu,Pia ujenzi wa Miundombinu ya maji."Mwigulu.
Hivyo wananchi wa Mbulu,Hakikisheni mnajitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura,na ichagueni CCM ikasimamie shughuli za maendeleo za jimbo la Mbulu Mjini na Vijijini.Wananchi wa Mbulu Mjini wakinyoosha mikono yao kuunga mkono ilani ya CCM na kuahidi kuichagua CCM kwenye Uchaguzi mkuu wa October 25.Kabla ya kufika Karatu Mjini,Mwigulu Nchemba alifanya mkutano kwenye kata ya mpakani mwa Mbulu Mjini na Vijijini.Katika mambo mengi anayozungumza Mwigulu Nchemba,Kubwa ameendelea kuwasihi Wananchi wafanye Uchaguzi wa Amani na Utulivu."Wananchi wa karatu,Kwanza nawapongezeni kwa ile hotuba ya Mzee wenu Dr.Slaa,Tunahitaji viongozi wanaosimama kwenye Maneno yao.Haiwezekani kwa miaka 20 wapinzani wamekuwa wakiimba kuwa Lowassa ni Fisadi,Lakini kwa sababu ya DILI,Siku moja wote wameamua kubaidlika na kumuunga mkono mtu aliyeliingiza Taifa hili kwenye Ufisadi mkubwa wa Richmond n.k.
Lakini kwa Dr.Slaa alionesha msimamo kama Mtanzania kuwa yeye si sehemu ya Ufisadi hivyo ataendelea kupinga Ufisadi ndio maana hakuwa tayari kumpokea Lowassa".
Mbali na hayo Mwigulu Nchemba ameendelea kuwasihi Watanzania kujitiokeza kupiga kura na Waichague CCM kwa maendeleo ya Karatu na Tanzania yote.Wananchi wa karatu Mjini wakifuatilia kwa Umakini Mkutano wa Mwigulu Nchemba.Mwigulu Nchemba aliwaasa watu wote wanaoamini katika Vurugu kuwa,Rais wa Tanzania atapatikana kwa kura kwenye sanduku la kupigia kura,Wanaolalamika kuwa wataibiwa kura ni wazi wanahofu kwasababu wameshashindwa kuanzia kusimamisha Mgombea hadi kwenye Uandaaji wa Ilani ya Uchaguzi.Kabla ya kuingia Mkoa wa Manyara,Mwigulu Nchemba mapema leo alizungumza na Wananchi wa kata ya Mitundu Jimbo la Manyoni Magharibi kuwaomba waichague CCM.
Picha na Sanga Festo Jr.

No comments:

Post a Comment