Tuesday, September 15, 2015

Mgombea Mwenza CCM Mama Samia Suluhu Hassan apukutisha Upinzani Lindi, 61 Wajiunga CCM, Wamo Viongozi

Umati wa wanaCCM na wapenzi wa chama hicho ukiwa umefurika katika uwanja wa Mnazi Mmoja nje kidogo ya mji wa Lindi Mjini kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu.
Umati wa wanaCCM na wapenzi wa chama hicho ukiwa umefurika katika uwanja wa Mnazi Mmoja nje kidogo ya mji wa Lindi Mjini kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu.
Umati wa wanaCCM na wapenzi wa chama hicho ukiwa umefurika katika uwanja wa Mnazi Mmoja nje kidogo ya mji wa Lindi Mjini kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu.
Mke wa Rais Kikwete, Mama Salma Kikwete akizungumza na umati wa wanaCCM na wapenzi wa chama hicho uliokuwa umefurika katika uwanja wa Mnazi Mmoja nje kidogo ya mji wa Lindi Mjini kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu.
Katibu, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akizungumza na wanaCCM na wananchi kwenye mkutano wa kampeni za mgombea mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu jana Mkoani Lindi.
Bi. Samia Suluhu (kulia) akimtambulisha mgombea mmoja wa wagombea udiwani katika Jimbo la Mchinga, kuzungumza na wapiga kura wa eneo hilo.
Samia Suluhu akimpokea mmoja wa wanachama mpya aliyejiunga na CCM katika Jimbo la Mchinga.

Bi. Samia Suluhu akimpokea mmoja wa wanachama mpya aliyejiunga na CCM katika Jimbo la Mchinga.
Mmoja wa wanachama wapya wa CCM aliyejiunga na CCM mara baada ya mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza katika Jimbo la Mchinga.
KAMPENI za mgombea mwenza wa nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu zinazoendelea mkoani Lindi zimekuwa tishio kwa vyama vya upinzani baada ya mkutano uliofanyika jana eneo la Mnazi Mmoja nje kidogo ya mji wa Lindi Mjini kuzoa wanachama 61 waliotoka upinzania na kujiunga na CCM.

Mkutano huo wa kampeni uliohudhuriwa pia na Mke wa Rais Mama Salima Kikwete umeacha maumivu kwa vyama vya upinzani vya CUF, Chadema na NCCR-Mageuzi baada ya kujikuta wanachama 61 wakivikimbia vyama vyao na kujikuta wakijiunga na Chama Cha Mapinduzi na kukabidhiwa kadi mpya za CCM kila mmoja.

Miongoni mwa wanachama ambao walipokelewa leo ni pamoja na Katibu wa Chadema Wilaya ya Lindi Mjini, Abdullah Madebe, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Mtaa wa Nananji Lindi, Bakari Kalulu na wanachama wengine kutoka vyama vya CUF na Chadema. Akizungumza baada ya kumkabidhi kadi, Bi. Samia Suluhu Katibu wa Chadema Wilaya ya Lindi Mjini alisema awali alipokuwa upinzani alikuwa amepotea na amegunduwa kuwa alikuwa anapoteza muda hivyo kuomba wananchi wamsamehe na ameamua kurudi kundini na kuendelea kulkijenga taifa.

Akizungumza baada ya kuwapokea wanachama hao, mgombea mwenza Suluhu alisema Serikali ya awamu ya tano imeandaa mambo mengi mazuri kwa mikoa ya Lindi na Mtwara na jambo la kwanza kulifanya baada ya kuunda serikali ni kuubadili mji wa Mtwara na Lindi kuwa miji ya viwanda, hali ambalo itakuza uchumi kwa kiasi kikubwa hivyo kunufaisa wananchi.

Alisema kwa kuanzia Serikali inajenga viwanda vinane mkoani Mtwara na vingine vitajengwa mkoani Lindi viwanda ambavyo vitategemea gesi katika uzalishaji wake bidhaa ambayo tayari inapatikana kwa wingi katika maeneo hayo. Alisema ujenzi wa viwanda utaongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na kuongeza nafasi za ajira jambo ambalo litawanufaisha wakazi wa eneo hilo na wawekezaji.

"...Tunataka kuitenga Lindi kuwa mji wa viwanda vitakavyoitumia gesi kwa uendeshaji, lengo ni kuwa na viwanda vitakavyozalisha nafasi za ajira takribani asailimia 40...," alisema Bi. Suluhu. Awali akihutubiwa katika mkutano wa kampeni ulofanyika Kata ya Mingumbi Kilwa Kusini, alisema Serikali inatambua hali ya kuyumba kwa soko la korosho na ufuta ili kukabiliana na hali hiyo imejipanga kujenga viwanda vya kubangua na kufunga korosho pamoja na kukamua mafuta kwa lengo la kumuongezea thamani mkulima katika zao analozalisha.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa Mnazi Mmoja Katibu, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye aliwatoa hofu akinamama na wapiga kura wengine juu ya vitisho vya kuwepo na vurugu kipindi cha uchaguzi kwa lengo la kuwatisha wapiga kura, hivyo kuwataka wananchi wasiogope kwani Serikali na CCM kupitia vijana wake imejipanga kupambana na wafanya fujo hao.

Alisema kitendo cha kutoa vitisho kwa wapiga kura ni kuibaka demokrasia hivyo CCM na vijana wake hawatakuwa tayari kuona demokrasia inabakwa nchini na wapuuzi wachahe. "...Vijana wa CCM naomba mkikamata kibaka wa demokrasia shughulikeni naye kidogo kabla ya kumpeleka polisi...CCM itashinda kwa kishindo," alisema Nape Nnauye.

Aidha msemaji huyo wa Chama Cha Mapinduzi alisema mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa pamoja na mpambe wake anayemuunga mkono Fredrick Sumaye hawawezi kuiponda Serikali ya CCM kwa kuwa wao wamekuwemo na kushika nafasi za juu za utendaji ndani ya serikali na kama walishindwa kuleta mabadiliko hawawezi kufanya hivyo leo.

Aliongeza kuwa kitendo cha kuendelea kuiponda ni sawa na kujidhalilisha wao wenyewe kwa wananchi hivyo kuwataka wasiwarubuni Watanzania kwamba wanamabadiliko ya msingi zaidi ya maslahi yao binafsi, ambayo ndiyo yanayowasukuma kukimbilia walipo.

Mgombea mwenza wa urais CCM, Bi. Suluhu bado anaendelea na ziara ya kuinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi Mkoani Lindi na baada ya kumaliza majimbo ya mkoa huo ataendelea katika Mkoa wa Mtwara, kuwashawishi wananchi kuichangua CCM ili iweze kupata ridhaa ya kuunda Serikali ya awamu ya tano.


Baadhi ya wanaCCM na wananchi wakiwa katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Suluhu kwenye Jimbo la 

Kutoka kushoto ni mgombea mwenza wa CCM nafasi ya uraisa, Bi. Samia Suluhu na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mwantumu Maiza na mgombea wa Jimbo la Mchinga Said Mtanda wakiwa kwenye mkutano wa kampeni katika Jimbo la Mchinga jana.
Mgombea Jimbo la Mchinga Said Mtanda akizungumza na wannaCCM na wananchi jana jimboni kwake ambapo mgombea mwenza alihutubia wananchi.
Sehemu ya wanaCCM na wananchi jana jimboni kwake ambapo mgombea mwenza alihutubia wananchi.
Mbunge wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dar es Salaam, Anjela Kiziga akizungumza katika mkutano wa kampeni za CCM. 
Aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Ushindi Chadema Taifa, Greison Nyakarungu ambaye kwa sasa amejiunga na CCM akizungumza katika moja ya mikutano ya kampeni ya CCM.
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Nkenge, Asumpta Mshama akipiga madongo kwa wapinzani kwenye moja ya mikutano ya kampeni ya CCM.  
Umati wa wanaCCM na wapenzi wa chama hicho ukiwa umefurika katika uwanja wa Mnazi Mmoja nje kidogo ya mji wa Lindi Mjini kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu.
Katibu, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bi. Mwantumu Mahiza.
Umati wa wanaCCM na wapenzi wa chama hicho ukiwa umefurika katika uwanja wa Mnazi Mmoja nje kidogo ya mji wa Lindi Mjini kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mwantumu Mahiza akizungumza na wanaCCM na wananchi kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu.
Mke wa Rais Kikwete, Mama Salma Kikwete, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Lindi, Mzee Ally Mtopa pamoja na mgombea mwenza wa CCM nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu wakijadiliana jambo kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa CCM viwanja vya Mnazi Mmoja.
Sehemu ya umati wa wanaCCM na wapenzi wa chama hicho ukiwa umefurika katika uwanja wa Mnazi Mmoja nje kidogo ya mji wa Lindi Mjini kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi, Bi. Samia Suluhu.
Katibu wa Chadema Wilaya ya Lindi Mjini, Abdullah Madebe akikabidhi kadi ya chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Aliyekuwa Katibu wa Chadema Wilaya ya Lindi Mjini, Abdullah Madebe (kulia) akipongezwa na Mgombea mwenza wa CCM nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu mara baada ya kujiunga na CCM, Katikati ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
Mmoja wa wananchi waliojiunga na CCM katika mkutano huo akizungumza baada ya kujiunga na chama hicho tawala.
Mmoja wa wananchi waliojiunga na CCM katika mkutano huo akizungumza baada ya kujiunga na chama hicho tawala.
Mama Salma Kikwete pamoja na Bi. Samia Suluhu wakipokea kadi za wanachama waliojiunga na CCM jana Mkoani Lindi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Lindi, Mzee Ally Mtopa kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa CCM viwanja vya Mnazi Mmoja.

Mgombea mwenza wa CCM nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu akizungumza na wanaCCM pamoja na wananchi viwanja vya Mnazi Mmoja.
Kada wa CCM na mbunge wa zamani wa Mchinga, Mudhir Mudhir akizungumza na wanaCCM pamoja na wananchi wa Jimbo la Mchinga katika mkutano wa kampeni.
*Imeandaliwa/www.thehabari.com

No comments:

Post a Comment