Wednesday, July 15, 2015

Binti wa Michuzi Achukua Form ya Ubunge wa Viti Maalum Tabora

 
 Zahara Michuzi alipowasili katika ofisi za CCM mkoa wa Tabora ili kuchukua form ya kugombea viti maalum kwa vijana.
Zahara Michuzi ni binti wa Issa Michuzi blogger na mpiga picha hodari wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye anamalizia muda wake sasa.
Binti wa Michuzi mara baada ya kuhitimu elimu yake ya shahada yake ya uchumi UDOM ameona ni vyema akawatumikia wananchi wa nyumbani kwake mkoani Tabora kwa kutangaza nia ya kugombea ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.
 Zahara Michuzi (kushoto) na Mwasham Hashim (kulia) karani wa UVCCM Tabora akitoa maelekezo ya uchukuaji wa form hizo.
 Binti huyo wa Michuzi akikabidhiwa form yake leo katika ofisi za UVCCM mkoa-Tabora
 Zahara akiifurahia form yake ya Ubunge wa viti maalum Tabora.
 Zahara (kushoto) akilipia fedha halali ya form hiyo huku mama yake mlezi (katikati) akishuhudia kitendo hicho.
 Zahara sasa safari yake ya kuufukuzia ubunge wa viti maalu ndipo ikaanza huku akiipitia form yake kwa mara ya kwanza toka azaliwe
Mwasham (kushoto) akitoa baadhi ya ufafanuzi kwa baadhi ya vipengele vilivyomo katika form hiyo.
Picha zote na aloyson.com TBN

No comments:

Post a Comment