Monday, October 19, 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AMNADI MBUNGE WA MUFINDI KASKAZINI MOHAMED MGIMWA





 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. MOhammed Gharib Bilal, akiwahutubia wananchi wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, mkoani Iringa wakati wa mkutano wa Kampeni za mgombea Ubunge wa jimbo hilo, Mohamed Mgimwa, uliofanyika juzi Okt 17.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya Viongozi wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, Mkoani Iringa wakati alipowasili Jimboni hapo juzi Okt 17, 2015 kwaajili ya kumnadi mgombea Ubunge wa Jimbo hilo, Mohamed Mgimwa.

 Baadhi ya Vijana wa CCM wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, wakiruka na kucheza staili ya mgombea Urais kupitia CCM, John Magufuli, wakati wa mkutano wa kampeni za mgombea Ubunge wa jimbo hilo, Mohamed Mgimwa, zilizofanyika mwishoni mwa wiki, jimboni hapo
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini, Mohamed Mgimwa, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika mwishoni mwa wiki jimboni humo
  Sehemu ya WanaCCM, waliojitokeza katika mkutano huo, wakimshangilia mgombea wao MOhamed Mgimwa wakati akitambulishwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya MUungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Mufundi Kaskazini, baada ya kumalizika kwa mkutano wa kampeni wa mgombea Ubunge wa Jimbo hilo, Mohamed Mgimwa. Picha na OMR

No comments:

Post a Comment