Monday, October 19, 2015

DKT FENELLA MUKANGARA AHAIDI KUTATUA TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA JIMBO LA KIBAMBA

  Umati wa wananchi wa kimara michungwani  wakimsikiliza mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi(CCM) Dkt Fenella Mukangara(hayupo pichani) wakati alipokuwa akinadi sera za chama chake jimboni kibamba.
 Mgombea Udiwani kata ya Saranga kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi(CCM) Bw.Haroun Yusuph Mdoe(kushoto) akizungumza  na wakazi wa Kimara Michungwani wakati wa kampeni za chama cha mapinduzi(CCM) jimbo la  kibamba.Kulia kwake ni Mgombea ubunge wa jimbo la kibamba kupitia chama hicho Dkt Fenella Mukangara.
 Mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi(CCM)  Dkt Fenella Mukangara akizungumza na wakazi wa kimara michungwani  wakati alipokuwa akinadi sera za chama chake.Dkt Fenella aliwaahidi wakazi hao kuwa wakimchagua atafanikisha kutatua suala la ajira kwa vijana ikiwemo kuwapa elimu ya ujasiriamali, kusimamia tatizo la maji,elimu na afya Bora.
Mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi(CCM)  Dkt Fenella Mukangara akipongezwa na baadhi ya wanachama wa chama hicho baada ya kumaliza mkutano wa kampeni  Kimara michungwani.

No comments:

Post a Comment