Sunday, December 1, 2019

DKT MUHAMMED SEIF KHATIB MTUNUKIWA WA KWANZA WA PhD CHUO KIKUU DODOMA

Na  Mwandishi wetu

Alipohojiwa mnamo January mwaka juzi, Dkt. Muhammed Seif  Khatib alikuwa na mengi ya kuzungumzia kuhusu umuhimu wa kuhifadhi historia, ambapo aliweka bayana kwamba wakati umefika wa kujenga makumbusho ya Taifa ya Mapinduzi ya Zanzibar, ili kizazi cha sasa na kijacho kiweze kujifunza na kuipitia historia muhimu kwa Watanzania na wageni kutoka nje.

Dkt. Khatib anasema ni vema kuonesha  katika  picha,  filamu,  maandishi  na  sura  halisi  za  historia  ya  Zanzibar ya wakati huo uliopita wa utawala wa wageni wa Waajemi, Wareno, Waarabu, Waingereza na hadi hivi sasa wakati wa Serikali ya Mapinduzi ya Waafrika inaongozwa na walio wengi. 

“Kwa kuweka makumbusho na usahihi wa historia ya nyuma ya kabla, wakati na baada ya Mapinduzi kadhalika na yanayotokea hivi sasa, hayo yote yakiwa katika makumbusho hio, yatakuwa msingi wa historia ya Zanzibar hatua ambayo itasaidia kuwekwa wazi mambo yaliyowahi kutokea, hivyo sio rahisi kwa mtu yoyote ambaye ana agenda ya kupotosha umma kufanya hivyo”,  alisema Dkt. Khatib ambaye unapokutana naye bado anaonekana ni mwenye nguvu zake na afya tele.

Ila kwa vile wazo lake la kuwa na kituo cha historia halijafanyiwa kazi, bado Dkt. Khatib tu anasikitika kwamba hivi sasa ni kweli kabisa mtu yoyote anaweza akasema vyovyote atakavyo kwa kuwa haijui historia vema na wala hana mahali pa kurejea historia ya Mapinduzi ya Zanzibar.  

“Wengi hawajui kwamba watu walitoka Kongo, Malawi, Kigoma na Tabora wakibebeshwa pembe za Ndovu na kusafiri kwa mguu, wakifuata njia ya reli ya kati, mpaka Bagamoyo na kusafirishwa na  jahazi  mpaka  Unguja  na  kuwekwa  sokoni  kuuzwa  kama  samaki  katika  soko  la watumwa. Huu ndio ukweli ambao sio tu wengi hawaujui, bali pia yapasa waujue” anasema Dkt. Khatib.

Anatoa  mfano  wa Rwanda  iliyokumbwa na  mauaji  ya  kimbari  mwaka  1994,  na kwamba kwa kutambua kuwa hicho siyo kitu kizuri kutokea tena hapa duniani nchi hiyo imeweka makumbusho ya kitaifa ambayo japo yanahuzunisha lakini ndio ukweli wenyewe. 

“Ukweli kwenye makumbusho hayo mjini Kigali utajionea maelfu ya mafuvu ya vichwa vya watu waliouwawa yalivyopangwa kiasi hata huwezi kuamini kama hiyo ndiyo iliyokuwa hali halisi ya mauaji ya kimbari yalivyotokea hapa duniani.

“Kwa Wanyarwanda na watu wengine duniani, makumbusho ya kimbari ni sehemu ya Utalii ikizingatia msemo wa waswahili wanasema kuona ni kuamini”, anasema Dkt. Khatib. 

Anaongeza kwamba siyo Rwanda tu, bali hata nchi ya Namibia kuna jumba la makumbusho la mauaji yaliyofanywa na Wajerumani kwa kabila la Waherero ambao anasema waliuwawa katika vita ya kwanza ya dunia, ambapo takribani Waherero nusu ya milioni waliuwawa na hivi karibuni Waherero wa Namibia walikuwa wanaomba fidia kwa Serikali ya Ujerumani, ingawa Ujerumani wameomba msamaha kwa mauaji hayo ya kimbari.

Dkt. Khatib anasema kwamba Uingereza ni nchi inayoongoza duniani kwa kuweka kumbukumbu zake katika makumbusho za kifalme, Kimataifa, Kitaifa, Vita, Silaha, Bahari, Mtu Binafsi, Jiji au Mji husika, ikiwa ina zaidi ya makumbusho 55 ambayo yanafahamika duniani. Mfano ikiwa ni British Museum London, Natural History Museum London, National Gallery London, Science Museum London, Victoria ana Albert Museum, National Maritime Museum, Museum of London City, National Portrait Gallery, National Army Museum, Sir Johns Soanes Museum, Wallace Collection London, National War Museum na kadhalika.

“Kujengwa kwa kituo cha makumbusho Zanzibar pia kitasaidia kuingiza fedha ikiwa kama sehemu ya Utalii wa historia kama wanavyofanya nchi zingine, ambapo mtu anayehitaji kuijua historia hiyo atapata kila kitu mahala pamoja bila kusumbuka”, anamalizia Dkt. Khatib.

Yote hayo tisa, mimi baada ya kufanya utafiti wa kina nikakuta kumbe hata yeye mwenyewe Dkt. Muhammed Seif Khatib ni mmoja wa watu ambao watafaa kuandikwa historia zao na kuwemo kwenye kituo hicho cha kumbukumbu, maana kwa kweli kapita kwingi na kufanya mengi na kuishi kwingi na kuona mengi.

Na endapo mtu akipata kibarua cha kuandika hiyo historia yake yeye kama yeye, hakika utapata taabu uanzie wapi ama fani ipi kati ya nyingi alizopitia na ambazo anazo hadi hii leo - kama ambavyo mimi nimepata shida kuandika hii sehemu tu ya historia yake hapa.

Baada ya kuongea nae kwa kina, nikawa najiuliza sijui nianze na hili jina la Daktari ambalo alilipata rasmi mnamo Novemba 25, 2011 pale alipotunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Dodoma na Mkuu wa Chuo hicho, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa.

“Hii ilikuwa Shahada ya Kwanza ya PhD kutoka katika Chuo Kikuu cha Dodoma. Ni bahati ilioje mimi kuipata Shahada hii ya juu kitaaluma” anasema Dkt. Khatib huku akiikumbuka vyema siku hiyo katika viwanja vya UDOM, wakati aliposimamishwa na kwenda kupiga goti na mbele ya Mhe. Mkapa na kutunukiwa Shahada hiyo.

Anasema Mada yake ya kuupata udaktari huo wa Falsafa ilikuwa ni ulinganisho wa washairi Shaaban Robert wa Tanga (wa karne ya 20) na Muyaka bin Haji wa Mombasa (wa karne ya 19), akichambua jinsi wanavyomsawiri mwanamke kwa “chanjo za matakwa ya mwanamume”. 

“Nilifarijika kufikia kiwango hicho cha elimu na kutunukiwa na Rais Mkapa ambaye niliyefanya kazi nae kwa muda wa miaka 10, akiamini kuwa mmoja wa mawaziri wake aliowaita “Askari wa Miamvuli”, anasema huku akitabasamu. 

Nikajiuliza labda nianze na historia yake ki-elimu, baada ya kuniambie yeye alisoma hadi darasa la nane lakini alijiendeleza mwenyewe na hatimaye kupata Shahada yake ya Kwanza,  katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1978 na Shahada ya Pili aliipata mwaka 1982 Uingereza SOAS. 

Kwa kweli Dkt. Khatib, ambaye baada ya kuhudumu kupitia Umoja wa Vijana kama mbunge wa viti maalumu baadaye akahudumu kama mbunge wa Uzini kwa miongo kadhaa, ni changamoto kubwa kumwelezea. 

Hasa ikizingatiwa kwamba yeye pia Mwenyekiti wa BARAZA LA KISWAHILI LA ZANZIBAR (BAKIZA), Mwenyekiti wa Mapitio ya Kamusi Fasaha la BAKITA lilochapwa 2010, huku akiwa Mhadhiri wa Muda kwa wanafunzi wa Shahada ya Uzamili (Masters) katika Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA). 

Na kama hayo yote hayatoshi, hivi karibuni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein alimteua kuwa Mjumbe wa TUME ya UTUMISHI WA UMMA katika Ofisi ya Rais, Zanzibar. 

Tukija alikokopita huko nyuma, utakuta Dkt. Khatib amewahi kushika nyadhifa nyingi na kwa muda mrefu ikiwa ni pamoja na  kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (1978-82), Katibu Mkuu Umoja huo (1982 - 88) ambapo hapo kwa vijana amekuwa kiongozi kwa miaka 10. 

Amekuwa Waziri katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu ya Pili ya Rais Ali Hassan Mwinyi, na awamu ya Tatu ya Mhe. Mkapa na ya nne ya Dkt. Jakaya Kikwete (1988-2010), safari hiyo akianzia toka akiwa mbunge wa viti vya Vijana na baadaye wa Jimbo la Uzini tokea mwaka 1988 hadi alipostaafu mwaka 2015. 

Vile vile amekuwa Mjumbe wa NEC ya CCM tokea 1978 hadi 2017, Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho (1995-2017), na baadaye Katibu wake wa  Oganaizesheni 2012-2017. 

Licha ya kuwa mwanasiasa mwenye nyadhifa mbalimbali, Dkt. Khatib katika muda wake wa ziada alikuwa mwandishi wa makala za michezo katika gazeti la Serikali la Daily News, gazeti la chama Uhuru na katika Mzalendo akiwika na makala yake mashuhuri KIPANGA. 

Na hakuishia magazetini pekee. Huyu bwana pia ni Mwandishi mashuhuri wa vitabu vikiwemo “Fungate ya Uhuru”, “Wasakatonge”, “Chanjo”, “Vifaru Weusi”, Utenzi wa Ukombozi wa Zanzibar” na “Taarab Zanzibar”. 

Nilipoongea nae hivi karibuni, Dkt. Khatib amenambia kwamba amehamasika sana na kitendo cha Mhe. Mkapa kutoa kitabu cha historia ya maisha yake, na kuongezea yeye pia tayari yuko mbioni kufuata nyayo za kiongozi huyo mahiri kwa kuandaa kitabu cha maisha yake. 

Hapana shaka kwamba kitabu chake hicho kitatuhadithia sio tu alivyokiuwa na kipawa cha kufanya mambo mengi kwa wakati  mmoja, bali pia jinsi alivyokuwa mwanasoka hodari wa timu ya Kikwajuni almaarufu kama “KISK” na timu ya Taifa ya Zanzibar - bila kusahau alikuwa pia Nahodha wa timu ya soka ya Chuo cha Nkrumah. 

Dkt. Khatibu, ambaye anasema hobby zake kubwa ni kufanya jogging, kusoma vitabu na makala mbaklimbali, pia ameshatunga nyimbo kibao za taarabu zinazoimbwa na wasanii wa bendi mbalimbali ikiwemo Culture.  Baadhi yake ni "Nia yangu sigeuzi", "Paka shume", "Wewe peke yako," "Nakupenda" na nyingine kibao.

Hadi nafikia hapa, bado sijajua nianzie wapi kumwelezea huyu mwanasiasa, mwanamichezo, mwanahabari, mshairi, ambaye kwa sasa  anasimamia kwa karibu kampuni ya familia ya Zanzibar Media Corporation akiwa Mkurugenzi wa Zenj Fm na Zenj Tv. 

Mie nashauri tusubiri tu hicho kitabu cha maisha yake ili tumjue kwa undani, na vile vile mamlaka zinazohusika, zikipendezwa, zianzishe hicho kituo cha kumbukumbu na historia ya Zanzibar kama anavyoshauiri - na kujumuisha kitabu chake kuwa miongoni mwa vitu vitavyowekwa humo.  Ama hakika, kwa maoni yangu, anastahili kuwemo kama ambavyo Wazanzibari wengi wa aina yake wanavyostahili.

 Dkt Muhammed Seif  Khatib aliposimamishwa ili kwenda kupiga goti Novemba 25, 2011 pale alipotunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Dodoma na Mkuu wa Chuo hicho, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa. Hii ilikuwa Shahada ya Kwanza ya PhD ya Chuo Kikuu cha Dodoma toka kianzishwe. 
 Dkt Muhammed Seif  Khatib  alipotunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Dodoma na Mkuu wa Chuo hicho, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa, Novemba 25, 2011. Hii ilikuwa Shahada ya Kwanza ya PhD ya Chuo Kikuu cha Dodoma toka kianzishwe.
 Dkt Muhammed Seif  Khatib katika tafrija ya kifamilia baada ya kutunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Dodoma na Mkuu wa Chuo hicho, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa, Novemba 25, 2011. Hii ilikuwa Shahada ya Kwanza ya PhD ya Chuo Kikuu cha Dodoma toka kianzishwe.
 Dkt Muhammed Seif  Khatib (namba 2) akiwa  na kikosi cha "Kiski" miaka ya 1970 
Akiwa Nahodha wa timu ya Chuo cha Nkrumah Dkt. Khatib akipokea kikombe cha ubingwa toka kwa Raisw wa kwanza wa Zanzaibar Sheikh Abeid Amnani Karume

 Dkt. Khatib akimkabidhi Mwalimu Nyerere Tunzo ya Kimataifa akiwa Katibu Mkuu wa Vijana mbele ya Rais Ali Hassan Mwinyi. Anasema hakumbuki mwaka ila kabla ya 1988

Dkt Muhammed Seif  Khatib wa pili kushoto waliosimama mbele. Hili lilikuwa baraza la mawaziri la kipindi cha pili cha Rais wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa. 
Dkt Muhammed Seif  Khatib akiwa katika majukumu yake kama Mkurugenzi wa Zanzibar Media Corporation Ltd., siku kilipoingia makubaliano ya kurusha vipindi vya CCTV ya China



Dkt Muhammed Seif  Khatib akiwa katika majukumu yake kama Mkurugenzi wa Zanzibar Media Corporation Ltd., akiwa na wageni waliotembelea Zenj FM/Zenj TV kutoka Amana Bank baadfa ya kufungua Tawi lao Zanzibar. Kutoka kulia ni Nassor Ameir, Dr.Muhammed Seif Khatib,Farsy Mussa na Jamal .I.Jamal
Ni Mwaka 2005  wakati Marehemu Ali Juma Shamuhuna alipokuwa mgeni wa Heshima katika ufunguzi wa Zenj FM.  Watatu kushoto ni Meneja wa  Zenj FM, Dkt. Khatib (kushoto), mwakilishi wa Mikunguni Mhe. SulShihata na Bwana Subash Patel.


Mwaka 1973 wakati Rais wa Zanzaibar wakati huo Mhe. Aboud Jumbe alipokutana na wajumbe wa Kamati ya kukusanya, kunakili na kuandika kitabu cha hotuba za Rais wa Kwanza wa Zanzibar Sheim Abeid Amani Karume. Dkt. Khatib ni wa tatu kutoka kushoto.
Dkt Khatib akiwa ofisini kwake na Omar Mkambara mtangazaji mahiri wa Soka kutoa BBC aliyekuwa katika maandalizi ya kutangaza mashindano ya AFCON  ' live' kutoka Misri na kupiga kambi Zenj FM  kuwashirikisha Wazanzibari.
Picha ya pamoja ya viongozi wa BAKITA na BAKIZA baada ya kikao cha mashauriano. Kutoka kulia waliosimama mbele ni Bi Mwanahija (Katibu Mtendaji - BAKIZA), Dkt.Muhammed Seif Khatib (Mwenyekiti - BAKIZA), Dkt.Sewangi (Katibu Mtendaji- BAKITA) na Dkt.Samwel ( Mwenyekiti - BAKITA) na wajumbe wengine.

Saturday, December 31, 2016

KAIMU KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA DKT. JUMA MALEWA AWAASA MAOFISA MAGEREZA KUTIMIZA WAJIBU WAO KWA UFANISI

Na Lucas Mboje, Dar es Saam
KAIMU Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa (pichani) amewaasa Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza  nchini kuzingatia  kuwa utendaji wao wa kazi za kila siku uende sambamba na kasi ya Serikali ya Awamu ya tano ili kuleta ufanisi unaotarajiwa.

KAIMU Kamishna Jenerali, Dkt. Malewa ameyasema hayo jana wakati wa Baraza la Kufunga Mwaka 2016 na kuukaribisha Mwaka 2017 lililowahusisha baadhi ya Maafisa na Askari kutoka Ofisi ya Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Ukonga, Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani pamoja na Magereza ya Mkoa wa D'Salaam.

Aidha, amewataka Maofisa na Askari wa Jeshi hilo kudumisha nidhamu wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kazi  ikiwemo kutekeleza mara moja Amri mbalimbali zinazotolewa na Viongozi wao wa Jeshi.
"Kila mmoja wenu atimize wajibu wake katika eneo lake la kazi kwa bidii, ari na moyo wa kujituma ili kuliwezesha Jeshi letu kupata ufanisi unaotarajiwa". Alisisitiza Kaimu Jenerali Dkt. Malewa.

Wakati huo huo Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa  pia ametumia fursa hiyo kuelezea baadhi ya mafanikio mbalimbali yaliyopatikana kwa Mwaka uliopita 2016 ambapo Jeshi la Magereza limeweza kupata jumla ya leseni 102 za uchimbaji wa madini ya ujenzi kama vile chokaa, mawe, kokoto, mchanga na Murram katika maeneo mbalimbali ya magereza. Pia katika mwaka 2016 Jeshi limeweza kujenga nyumba 129 kwa njia ya kujitolea ambapo nyumba 231 zipo katika hatua mbalimbali ya ukamilishaji. 

Aidha, Ujenzi wa nyumba 320 za makazi ya askari katika eneo la Gereza Ukonga maandalizi ya ujenzi yanaendelea na ujenzi wa nyumba hizo ni kufuatia ziara ya Rais Magufuli  Novemba 29 mwaka huu  ambapo alipokea taarifa ya uhaba wa nyumba za kuishi askari wa jeshi hilo na akaagiza Jeshi la Magereza lipatiwe Tsh. bilioni 10 haraka ili kupunguza tatizo hilo.
Shirika la Magereza na Mfuko wa hifadhi ya Jamii wa PPF wameingia Makubaliano ya Mkataba wa ubia katika mradi wa ujenzi wa Kiwanda kipya cha kusakata ngozi pamoja na uwekezaji wa mashine za kisasa za kutengnezea bidhaa za ngozi katika Kiwanda cha Viatu cha Gereza Karanga, Moshi.

Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga kimepata Ithibati na hivyo kuwa na hadhi ya kuwa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji na mapema mwakani kinatarajia kudahili wanafunzi 30 katika fani ya Taaluma ya Urekebishaji ngazi ya cheti.  
Pamoja na Mafanikio hayo, Kaimu Kamishna Jenerali Dkt. Malewa ameelezea changamoto mbalimbali zinazolikabili Jeshi hilo ikiwemo ufinyu wa bajeti, makazi duni ya maofisa na askari, uhaba wa vitendea kazi, ukosefu wa pembejeo pamoja na madeni ya wabuni na watumishi wa jeshi hilo. 
Kuhusu maeneo yatakayopewa kipaumbele kwa Mwaka mpya 2017 ni kuwa Jeshi la Magereza litaendeleza jitihada za kuimarisha na kuongeza uzalishaji kwenye miradi ya uzalishaji wa mazao ya Kilimo na mifugo lengo ikiwa ni kujitosheleza kwenye chakula cha wafungwa, kuhakikisha wafungwa wanafanya kazi za uzalishaji mali kwa kiwango chenye tija badala ya kukaa tu magerezani pia kuendeleza mikakati ya kupunguza msongamano magerezani.
Baraza la kufunga Mwaka na kuukaribisha Mwaka unaofuata ni utamaduni wa siku nyingi ambao unaenziwa na Viongozi Wakuu wa Jeshi la Magereza ambapo Baraza la aina hii hufanyika kila Mwaka ili Kamishna Jenerali wa Magereza nchini aweze kuongea na Watumishi wote wa Jeshi la Magereza nchini kupitia Baraza hilo lengo ikiwa ni kufanya tathmini ya yale yaliyojiri katika Jeshi kwa kipindi cha Mwaka unaisha kwa kuzungumzia mafanikio na changamoto zilizojitokeza na  kutazama matarajio ya Mwaka mpya.

Monday, March 21, 2016

PPF KANDA YA ZIWA IMEWAFIKISHA WAAJIRI SABA MAHAKAMANI KWASHINDWA KULETA MCHANGOYAO.

MENEJA MFUKO WA HIFADHI ZA JAMII PPF KANDA YA ZIWA, MESHACK BANDAWE, AMEWAFIKISHA MAHAMANI WAAJIRI SABA KWAKUSHINDWA KULETA MICHANGO YA WATUMISHIWAO.

AKIONGEA KATIKA SEMINA HIYO NA WAAJIRI WATAASISI MBALIMBALI JIJINI MWANZA BW.MESHACK BANDAWE,FAIDA ZINAZOTOLEWA NA MFUKO WA HIFADHI ZA JAMII KANDA YA ZIWA ALISEMA MFUKO WA HIFADHI ZA JAMII UMEFANIKIWA KUKUSANYA ZAIDI YA BILIONI TISA.AMBAPO PIA WAMEFANIKIWA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI WAAJIRI SABA WALIOSHINDWA KUWAKILISHA MICHANGO YAO YA ZAIDI MILIONI 500.

KATIKA SEMINA HIYO MENEJA WA MFUKO WA HIFADHI ZA JAMII AMESEMA HAYUKO TAYARI KUMFIKISHA MAHAKAMANI MUAJIRI YOYOTE ENDAPO TU ATATEKELEZA WAJIBUWAKE.

PIA AMEWAMBA WAJIRI WAACHE KABISA KUCHELEWESHA MICHANGO KWANI NIHAKIYAMSINGI KUPELEKA MICHANGO KWANI WATUMISHIWAO WANAWAFANYIKA WAWEZEKUPATA MAFAO YAO KWAWAKATI.
Baadhi ya wateja wakichangia hoja  katika semina hiyo.
 bi.Happines Manyenye,akitoa maswali kwawateja wake wa mfuko wa PPF jijini Mwanza.

 Bw.Mashack Bandawe,meneja wa PPF kanda ya ziwa akieleza faida za mfuko wa hifadhi za jamii PPF jijini Mwanza.
Maafisa wa mfuko wa ppf wakiwa kwenye semina jijini Mwanza. 
Meshack Bandawe akionyesha huduma mbalimbali PPF inazozitoa hapa nchini. 







 Taasisi mbalimbali wakiwa katika semina iliyoandaliwa na PPF.

Sunday, January 17, 2016

SIMU TV: HABARI KUTOKA VITUO VYA TELEVISHENI

Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Nape Nnauye alifuta gazeti la Mawio kwa tuhuma za kuandika habari za kichochezi.https://youtu.be/3sBeUgEn4RI

Waumini wa dini kiislamu nchini watakiwa kuunga mkono juhudi za serikali katika mapambano ya dhidi ya rushwa na ufisadi.https://youtu.be/Yh0oQLChKBA

Jeshi la polisi mkoani Iringa linawashikilia watu 85 wanaosadikiwa kuwa raia wa Ethiopia kwa tuhuma za kuingia nchini bila vibali.https://youtu.be/XtwMPLCOjIg

Serikali yatangaza kusitisha uuzwaji wa nyumba zake ilizopangisha kupitia shirika la nyumba NHC amabazo hazipo kwenye miradi ya nyumba za mauzo ili kuhakikisha wananchi wa kipato cha chini wanaendelea kusaidiwa na serikali.https://youtu.be/6SKDPhV389M

Wakazi 45 wa mtaa wa Kchangani kata ya Majohe manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam wafanikiwa kupimiwa makazi yao na kupata hatimiliki ya makazi.https://youtu.be/enKlC6n2SDs

Kilio cha wachimbaji wadogo wa Madini katika halmashauri ya wilaya Chunya mkoani Mbeya kwa Rais Magufuli kuwasaidia eneo la uchimbaji chapata ufumbuzi baada ya serikali kuuamuru mmiliki wa mgodi wa Shanta kuondoka na kuwaachia wananchi. https://youtu.be/3SWT6C_fTcU  

BOT yaipa siku 20 benki ya Stanbic ya hapa nchini kujitetea kwanini isichukuliwe hatua kwa kufanya miamala yenye mashaka.https://youtu.be/-2W2KwJwp9U

Bunge la Jumuiya ya Afika Mashariki lauvalia njuga mgogoro wa Burundi huku kamati ya jumuiya ya EAC inayoshughulika na mgogoro ikitaka kukutana na serikali ya Burundi. https://youtu.be/PvQpDM5BNdE

Baraza la vijana la Chadema BAVICHA latishia kumshitaki msajili wa vyama nchini kama hatokichukulia hatua chama cha mapinduzi hatua za kinidhamu kufuatia wafuasi wa chama hicho kutoa ujumbe wa kibaguzi.https://youtu.be/Ko7eit5P9OA

Migogoro sekta ya ardhi yaendelea kuwa kaa la moto hapa nchini baada ya mtu mmoja kuuwawa na nyumba 44 kuchomwa moto kufuatia mgogoro wa ardhi wilayani Muleba mkoani Kagera. https://youtu.be/tDI9thnyA0A

Serikali yapiga marufuku kwa watendaji wa maliasili nchini kuharibu mali za wananchi waliovamia maeneo ya hifadhi na badala yake kutoa elimu kuhusu sheria ya misitu kwa wananchi. https://youtu.be/NxgSNZ4kJNQ  

Benki kuu ya Tanzania yaiandikia barua benki ya Stanbic Tanzania kwa lengo la kuitoza faini baada ya kubaini miamara ya kutia shaka;https://youtu.be/QstLeQBXaJs  

Serikali wilayani Kasulu mkoani Kigoma imewataka walimu kurejesha fedha walizowachangisha wazazi wakati wa kuwaandikisha watoto shuleni;https://youtu.be/DhKMmOCYe4Q   

Mbunge wa jimbo la Segerea kwa tiketi ya CCM, Mhe. Bonna Kaluwa amezindua kampeni kwa lengo la kuboresha miundombinu ya shule na utoaji wa elimu bora  kwa wanafunzi; https://youtu.be/xrg4CCrvj0M  

Serikali imelifuta gazeti la Mawio katika daftari la usajili wa magazeti kutokana na kukiuka sheria ya vyombo vya habari; https://youtu.be/4LknCRI1iAk  

Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi aigiza serikali mkoani Morogoro kupitia upya orodha ya mashamba makubwa yaliyowekwa rehani ili kujiridhisha kama yanaendelezwa; https://youtu.be/KOgJdfSfJog  

Timu ya Yanga yamaliza mgogoro uliokuwepo baina yake na mchezaji wa kimataifa Haruna Niyonzima baada ya kukiri kosa na kuomba msamaha;https://youtu.be/T4nFy1vwohY  

Timu ya Yanga imeibuka na ushindi wa goli 1 kwa 0 dhidi ya timu ya Ndanda ya mkoani mtwara katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara;https://youtu.be/0TeGBPCTmpQ  

Serikali yavitoza faini viwanda viwili vya mkoani Morogoro kwa kukiuka sheria ya mazingira; https://youtu.be/DnHE3lSjWxw
    
Waziri wa kilimo,mifugo na uvuvi, Mhe. Mwigulu Nchemba awachukulia hatua kali watendaji wa serikali na mawakala wa pembejeo mkoani Ruvuma kwa tuhuma ya udanganyifu; https://youtu.be/YYerUPkMWrc  

Serikali wilayani Hai mkoani Kilimanjaro yazifunga kambi za wakulima kufutia kulipuka kwa ugonjwa wa kipindupindu wilayani humo;https://youtu.be/oB5zo9qTF4I  

Baadhi ya wanafunzi wenye ulemavu katika shule ya wasichana ya Rugambwa  mkoani Kagera wameiomba serikali na wadau kuwasaidia ujenzi wa miondombinu rafiki itakayozingatia mahitaji ya wanafunzi wenye ulemavu;https://youtu.be/WFfyq8CRP2w   

inaelezwa kuwa serikali imeanza kuangalia upya viwango vya kodi katika shirika la nyumba la taifa NHC; https://youtu.be/iuaYSiPRZgw  

Baadhi ya mashabiki wa timu ya Simba waelezea maoni yao kuhusu kiwango kinachooneshwa na timu yao; https://youtu.be/KZKmVJJZj88  

Kocha wa timu ya Everton, Roberto Martinez alalamikia goli lililofungwa na mchezaji wa Chelsea, John Terry kuwa lilikuwa la kuotea;https://youtu.be/WV8gOJrP-m8

Monday, November 2, 2015

TAWI LA CCM EMPRESS KWA FUNDI MUSA MTAA WA SAMORA WASHEREHEKEA USHINDI WA DK. JOHN POMBE MAGUFULI

1
MBUNGE mteule wa Muleba Kaskazini (CCM) na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Mwijage akisalimiana na Godson Kaligo Mjumbe wa tawi la CCM Epress Social lililopo mtaa wa Samora maarufu kwa Musa Shoeshine alipowatembelea wakati wa sherehe yao ya kusherehekea ushindi wa Rais Mteule Dr. John Pombe Magufuli mara baada ya kushinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu nchini kote, Wana CCM hao wamesherehekea kwa muziki na kupata supu ya mbuzi na nyama choma huku wakiwakaribisha wananchi mbalimbali bila kujali itikadi zao kwani Dr John Pombe Magufuli ni Rais wa Watazania wote.(PICHA NA RASHID SHOTI-DAR ES SALAAM)
3
MBUNGE mteule wa Muleba Kasikazini (CCM) na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Charles Mwijage akibadilishana mawazio na Godson Kaligo na wana CCM wa tawi hilo.
4
Katibu wa Tawi hilo Musa Mtulia ambaye pia ni Shoeshine Maarufu mtaa wa Samora akiendelea na kazi yake huku wana CCM wengine na wadau wengine wakiendelea na sherehe hiyo kwa kupata supu.
5
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa tawi hilo Hassan Mneo. Mjumbe Godson Kaligo pamja na wadau wengine wakipata supu kutoka kulia ni Bw. Haogwa na Mzee Mnonji shabiki maarufu wa timu ya Simba.
6
Mwana CCM Richard Wambura aliyesimama nyuma naye alijumuika na wana CCM wenzake wakati alipowatembelea tawini hapo
7
Hapa ni mwendo wa kutafuna mbuzi tu.
9
Mwenyekiti Hassan Mneo kushoto na we nzake wakipata supu na kahawa katika wtawi hilo
10Katibu wa tawi Musa Mtulia akifurahi na wadau mbalimbali waliofika katika tawi hilo wakati wa sherehe hiyo.

Tuesday, October 27, 2015

WILFRED LWAKATARE WA CHADEMA AIBUKA KIDEDEA UBUNGE BUKOBA MJINI

Hatimaye Mkurugenzi wa ulinzi na usalama wa chama cha demokrasia na maendeleo -Chadema Bw. Wilfred Lwakatare ameibuka kidedea leo hii kuwa Mbunge wa Bukoba Mjini akiibuka kidedea dhidi ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini kwa tiketi ya CCM, Khamis Kagasheki. Matokeo hayo yametanga usiku huu punde na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Bukoba mjini Bw. Aron T. Kagurumjuli. Kura za Udiwani Chadema/ Ukawa imeshinda Kata zifuatazo: Kahororo, Kagondo, Kibeta, Kitendaguro, Nshambya, Hamugebe, Kashai, Bakoba na Bilele. CCM imepata Kata ya Rwamishenye, Buhembe, Miembeni, Nyanga na Ijunganyondo. 

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Bukoba mjini Bw. Aron T. Kagurumjuli akitoa matokeo usiku wa kuamkia leo saa 2:30 na kumtangaza Lwakatare kwamba ndie mshindi na Nafasi hiyo ya Ubunge Bukoba Mjini. 
Bw. Aron T. Kagurumjuli(Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Bukoba mjini) akiendelea na zoezi la kutangaza matokeo usiku huu.
Mshindi wa nafasi ya Ubunge wa Bukoba Mjini Bw. Wilfred Lwakatare kupitia Chama cha CHADEMA akifurahia baada ya kuibuka kidedea katika kinyang'anyiro hicho baada ya kumwangusha mgombea mwenza aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo la Bukoba Mjini kwa tiketi ya CCM, Khamis Sued Kagasheki usiku huu. Picha na Faustine Ruta, Bukoba


Licha ya kuonekana kana kwamba hapakuwa na dalili zozote za fujo wakati wa zoezi la upigaji kura za Ubunge na udiwani, hali ilibadilika  jumatatu asubuhi baada ya wafuasi wa chama cha Chadema kutaka matokeo mapema baada ya kupata matokeo hayo usiku wa kuamkia leo hii kuwa Chadema imeshinda katika Kata 9 kati ya 14 wafuasi hao waliandamana katika maeneo ya mji wa Bukoba wakitaka majibu yatolewe mapema. Kitu ambacho hakikufanyika na Jioni hii kuleta kasheshe na ghasia. Hali hiyo ilisababisha polisi wa kutuliza ghasia kuingilia kati na kuwatawanya vijana hao ambao mpaka usiku  walikuwa wamepandwa na jazba katika eneo la ofisi za Halmashauri ya Bukoba. Vurugu zikiwemo kurushiana mawe zilitokea. Ndipo polisi walitumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi waliokusanyika katika Ofisi za Halmashauri na kuanza kurusha mawe wakishinikiza kutangazwa kwa matokeo ya ubunge. Hali hiyo ilitulia baada ya Viongozi wa Chadema kuwatuliza na ndipo Matokeo yakatangazwa. 
Taarifa zinasema kuwa kulikuwa na mchuano mkali kati ya wagombea hao wawili ambao ni Wilfred Lwakatare wa chama cha Chadema na aliyekuwa Mbunge wa Bukoba Mjini kupitia chama cha CCM Khamis Sued Kagasheki. Kitu kilichopelekea kurudiwa kuhesabiwa kwa kura zote na kupata uhakika wa kutosha.

Kura zilizokubalika ni 54,211 sawa na asilimia 98.54, kura zilizoharibika ni 805 sawa asilimia 1.46, Matokeo ni kama ifuatavyo TLP kura 81 sawa na asilimia 0.2, ACT kura 453, Khamis Sued Kagasheki wa CCM amepata kura 25,565 sawa na asilimia 47.2, Wilfred Lwakatare wa Chadema amepata kura 28,112 sawa na asilimia 51.9Wafuasi wa Chadema walionekana wakiwa wamekusanyika katika Ofisi za Halmashauri Bukoba wakidai kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa huo wa Wabunge.
Vingozi wa Chama cha Chadema wakiteta jambo, kushoto) ni Bw. Chief Kalumuna Mshindi wa Udiwani Kata ya Kahororo aliyeshinda kiti hicho katika Uchaguzi huu wa 2015. (Kulia) ni Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema wilaya ya Bukoba Victor Sherejei.
Bw. Wilfred Lwakatare kupitia Chama cha CHADEMA akiteta jambo na Diwani wa Kata ya Kahororo kupitia Chama cha Chadema katika Ofisi za Halmashauri ya Bukoba mjini huku wakisubiri matokeo ya Ubunge Bukoba Mjini.
Bw. Wilfred Lwakatare kupitia Chama cha CHADEMA
Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema wilaya ya Bukoba Victor Sherejei (kulia) mbele akiteta na Chief Kalumuna Diwani wa kata kahororo wakibadilisha mawazo wakati wakisubiri matokeo usiku huu.Waandishi wa habari na Makada wa Chama cha Chadema wakiwa katika Ofisi za Halmashauri ya Bukoba
Kidedea...Chif Kalumuna(kulia) wa Kata ya Kahororo akiwa amembeba mshindi bw. Wilfred Lwakatare
Wafuasi wa Chadema walionekana wakiwa wamekusanyika kutaka kuvamia Ofisi za Halmashauri ya Bukoba kudai kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa wabunge na Polisi walikuwa tayari kuwakabili vilivyo na kuzuia umati huo mkubwa.
Wafuasi wa Chadema wakitaka Matokeo yatolewa baada ya kuchukuwa muda tangu asubuhi mpaka jioni hii.
Taswira jioni hii maeneo ya karibu na Ofisi za Halmashauri.
Hapa ikabidi kiongozi wa Chadema aliyeshinda katika Kata ya Kashai kupitia chama hicho awatulize kwamba matokeo yanaenda kutolewa jioni hii.
Wafuasi wa Chadema wakitaka Matokeo
Wafuasi wa Chadema wakitaka Matokeo ya Kiongozi wao.