Sunday, January 17, 2016

SIMU TV: HABARI KUTOKA VITUO VYA TELEVISHENI

Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Nape Nnauye alifuta gazeti la Mawio kwa tuhuma za kuandika habari za kichochezi.https://youtu.be/3sBeUgEn4RI

Waumini wa dini kiislamu nchini watakiwa kuunga mkono juhudi za serikali katika mapambano ya dhidi ya rushwa na ufisadi.https://youtu.be/Yh0oQLChKBA

Jeshi la polisi mkoani Iringa linawashikilia watu 85 wanaosadikiwa kuwa raia wa Ethiopia kwa tuhuma za kuingia nchini bila vibali.https://youtu.be/XtwMPLCOjIg

Serikali yatangaza kusitisha uuzwaji wa nyumba zake ilizopangisha kupitia shirika la nyumba NHC amabazo hazipo kwenye miradi ya nyumba za mauzo ili kuhakikisha wananchi wa kipato cha chini wanaendelea kusaidiwa na serikali.https://youtu.be/6SKDPhV389M

Wakazi 45 wa mtaa wa Kchangani kata ya Majohe manispaa ya Ilala jijini Dar es salaam wafanikiwa kupimiwa makazi yao na kupata hatimiliki ya makazi.https://youtu.be/enKlC6n2SDs

Kilio cha wachimbaji wadogo wa Madini katika halmashauri ya wilaya Chunya mkoani Mbeya kwa Rais Magufuli kuwasaidia eneo la uchimbaji chapata ufumbuzi baada ya serikali kuuamuru mmiliki wa mgodi wa Shanta kuondoka na kuwaachia wananchi. https://youtu.be/3SWT6C_fTcU  

BOT yaipa siku 20 benki ya Stanbic ya hapa nchini kujitetea kwanini isichukuliwe hatua kwa kufanya miamala yenye mashaka.https://youtu.be/-2W2KwJwp9U

Bunge la Jumuiya ya Afika Mashariki lauvalia njuga mgogoro wa Burundi huku kamati ya jumuiya ya EAC inayoshughulika na mgogoro ikitaka kukutana na serikali ya Burundi. https://youtu.be/PvQpDM5BNdE

Baraza la vijana la Chadema BAVICHA latishia kumshitaki msajili wa vyama nchini kama hatokichukulia hatua chama cha mapinduzi hatua za kinidhamu kufuatia wafuasi wa chama hicho kutoa ujumbe wa kibaguzi.https://youtu.be/Ko7eit5P9OA

Migogoro sekta ya ardhi yaendelea kuwa kaa la moto hapa nchini baada ya mtu mmoja kuuwawa na nyumba 44 kuchomwa moto kufuatia mgogoro wa ardhi wilayani Muleba mkoani Kagera. https://youtu.be/tDI9thnyA0A

Serikali yapiga marufuku kwa watendaji wa maliasili nchini kuharibu mali za wananchi waliovamia maeneo ya hifadhi na badala yake kutoa elimu kuhusu sheria ya misitu kwa wananchi. https://youtu.be/NxgSNZ4kJNQ  

Benki kuu ya Tanzania yaiandikia barua benki ya Stanbic Tanzania kwa lengo la kuitoza faini baada ya kubaini miamara ya kutia shaka;https://youtu.be/QstLeQBXaJs  

Serikali wilayani Kasulu mkoani Kigoma imewataka walimu kurejesha fedha walizowachangisha wazazi wakati wa kuwaandikisha watoto shuleni;https://youtu.be/DhKMmOCYe4Q   

Mbunge wa jimbo la Segerea kwa tiketi ya CCM, Mhe. Bonna Kaluwa amezindua kampeni kwa lengo la kuboresha miundombinu ya shule na utoaji wa elimu bora  kwa wanafunzi; https://youtu.be/xrg4CCrvj0M  

Serikali imelifuta gazeti la Mawio katika daftari la usajili wa magazeti kutokana na kukiuka sheria ya vyombo vya habari; https://youtu.be/4LknCRI1iAk  

Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi aigiza serikali mkoani Morogoro kupitia upya orodha ya mashamba makubwa yaliyowekwa rehani ili kujiridhisha kama yanaendelezwa; https://youtu.be/KOgJdfSfJog  

Timu ya Yanga yamaliza mgogoro uliokuwepo baina yake na mchezaji wa kimataifa Haruna Niyonzima baada ya kukiri kosa na kuomba msamaha;https://youtu.be/T4nFy1vwohY  

Timu ya Yanga imeibuka na ushindi wa goli 1 kwa 0 dhidi ya timu ya Ndanda ya mkoani mtwara katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara;https://youtu.be/0TeGBPCTmpQ  

Serikali yavitoza faini viwanda viwili vya mkoani Morogoro kwa kukiuka sheria ya mazingira; https://youtu.be/DnHE3lSjWxw
    
Waziri wa kilimo,mifugo na uvuvi, Mhe. Mwigulu Nchemba awachukulia hatua kali watendaji wa serikali na mawakala wa pembejeo mkoani Ruvuma kwa tuhuma ya udanganyifu; https://youtu.be/YYerUPkMWrc  

Serikali wilayani Hai mkoani Kilimanjaro yazifunga kambi za wakulima kufutia kulipuka kwa ugonjwa wa kipindupindu wilayani humo;https://youtu.be/oB5zo9qTF4I  

Baadhi ya wanafunzi wenye ulemavu katika shule ya wasichana ya Rugambwa  mkoani Kagera wameiomba serikali na wadau kuwasaidia ujenzi wa miondombinu rafiki itakayozingatia mahitaji ya wanafunzi wenye ulemavu;https://youtu.be/WFfyq8CRP2w   

inaelezwa kuwa serikali imeanza kuangalia upya viwango vya kodi katika shirika la nyumba la taifa NHC; https://youtu.be/iuaYSiPRZgw  

Baadhi ya mashabiki wa timu ya Simba waelezea maoni yao kuhusu kiwango kinachooneshwa na timu yao; https://youtu.be/KZKmVJJZj88  

Kocha wa timu ya Everton, Roberto Martinez alalamikia goli lililofungwa na mchezaji wa Chelsea, John Terry kuwa lilikuwa la kuotea;https://youtu.be/WV8gOJrP-m8